< Zaburi 22 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
To the Chief Musician. On "the Hind of the Dawn." A Melody of David. My GOD, my GOD, why hast thou forsaken me? Far from saving me, The words of my loud lamentation?
2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
My God! I keep crying—By day, and thou dost not answer, and, By night, and there is no rest for me.
3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
But, thou, art holy, Who inhabitest the praises of Israel.
4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
In thee, trusted our fathers, They trusted, and thou didst deliver them;
5 Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
Unto thee, made they outcry, and escaped, In thee, they trusted, and had not turned pale.
6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
But, I, am a worm and no one, a reproach of men, and despised of a people;
7 Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
All that see me, laugh at me, —They open wide the mouth, They shake the head: —
8 Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
He should trust in Yahweh—let him deliver him, —Let him rescue him, seeing he delighteth in him.
9 Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
For, thou, art he that severed me from the womb, he that caused me to trust, upon the breasts of my mother;
10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
Upon thee, was I cast from the time I was born, From the womb of my mother, my GOD, hast thou been.
11 Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
Be not far from me, for, distress, is near, For there is none to help.
12 Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
Many bulls have surrounded me, Strong oxen of Bashan, have enclosed me;
13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
They have opened wide against me their mouth, A lion rending and roaring.
14 Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
Like water, am I poured out, and, put out of joint, are all my bones, —My heart, hath become, like wax, it is melted in the midst of my body;
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
Dried as a potsherd, is my strength, And, my tongue, is made to cleave to my gums, And, in the dust of death, wilt thou lay me.
16 Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
For dogs have surrounded me, —An assembly of evil doers, have encircled me, They have pierced my hands and my feet,
17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
I may tell all my bones, They, look for—they behold me!
18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
They part my garments among them, and, for my vestment, they cast lots.
19 Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
But, thou, O Yahweh, be not far off, O my help! to aid me, make haste;
20 Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
Rescue, from the sword, my life, from the power of the dog, my solitary self:
21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
Save me from the mouth of the lion, —Yea, from the horns of wild beasts, hast thou delivered me.
22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
I will declare thy Name unto my brethren, —In the midst of the convocation, will I praise thee.
23 Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
Ye that revere Yahweh, praise him, All ye the seed of Jacob, glorify him, And, stand in awe of him, all ye seed of Israel.
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
For he hath not despised nor abhorred the humbling of the patient one, neither hath he hid his face from him, but, when he cried for help unto him, he heard.
25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
Of thee, is my praise in the great convocation, My vows, will I pay, before them who revere him.
26 Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
The patient wronged-ones shall eat and be satisfied, They shall praise Yahweh, who are seekers of him, Let your heart live for aye.
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
All the ends of the earth, will remember and turn to Yahweh, Yea all the families of the nations, will bow themselves down before thee,
28 kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
For, to Yahweh, belongeth the kingdom, And One to Rule over the nations.
29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
All the great ones of the earth, shall eat and bow down, Before him shall kneel, all that go down to the dust, Even he who had not kept alive, his own soul!
30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
My seed, shall serve him, It shall be recounted, of the Lord, to a generation that shall come:
31 Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.
That his righteousness may be declared to a people to be born, That he wrought with effect!