< Zaburi 22 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
For the Chief Musician; set to Aijeleth hash-Shahar. A Psalm of David. My God, my God, why hast thou forsaken me? [why art thou so] far from helping me, [and from] the words of my roaring?
2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
O my God, I cry in the day-time, but thou answerest not; and in the night season, and am not silent.
3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
But thou art holy, O thou that inhabitest the praises of Israel.
4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
Our fathers trusted in thee: they trusted, and thou didst deliver them.
5 Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
They cried unto thee, and were delivered: they trusted in thee, and were not ashamed.
6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
But I am a worm, and no man; a reproach of men, and despised of the people.
7 Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
All they that see me laugh me to scorn: they shoot out the lip, they shake the head, [saying],
8 Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
Commit [thyself] unto the LORD; let him deliver him: let him deliver him, seeing he delighteth in him.
9 Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
But thou art he that took me out the womb: thou didst make me trust [when I was] upon my mother’s breasts.
10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
I was cast upon thee from the womb: thou art my God from my mother’s belly.
11 Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
Be not far from me; for trouble is near; for there is none to help.
12 Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
Many bulls have compassed me: strong bulls of Bashan have beset me round.
13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
They gape upon me with their mouth, [as] a ravening and a roaring lion.
14 Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
I am poured out like water, and all my bones are out of joint: my heart is like wax; it is melted in the midst of my bowels.
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
My Strength is dried up like a potsherd; and my tongue cleaveth to my jaws; and thou hast brought me into the dust of death.
16 Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
For dogs have compassed me: the assembly of evil-doers have enclosed me; they pierced my hands and my feet.
17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
I may tell all my bones; they look and stare upon me:
18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
They part my garments among them, and upon my vesture do they cast lots.
19 Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
But be not thou far off, O LORD: O thou my succour, haste thee to help me.
20 Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
Deliver my soul from the sword; my darling from the power of the dog;
21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
Save me from the lion’s mouth; yea, from the horns of the wild-oxen thou hast answered me.
22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
I will declare thy name unto my brethren: in the midst of the congregation will I praise thee.
23 Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
Ye that fear the LORD, praise him; all ye the seed of Jacob, glorify him; and stand in awe of him, all ye the seed of Israel.
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
For he hath not despised nor abhorred the affliction of the afflicted; neither hath he hid his face from him; but when he cried unto him, he heard.
25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
Of thee cometh my praise in the great congregation: I will pay my vows before them that fear him.
26 Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
The meek shall eat and be satisfied: they shall praise the LORD that seek after him: let your heart live for ever.
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
All the ends of the earth shall remember and turn unto the LORD: and all the kindreds of the nations shall worship before thee.
28 kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
For the kingdom is the LORD’S: and he is the ruler over the nations.
29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
All the fat ones of the earth shall eat and worship: all they that go down to the dust shall bow before him, even he that cannot keep his soul alive.
30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
A seed shall serve him; it shall be told of the Lord unto the [next] generation.
31 Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.
They shall come and shall declare his righteousness unto a people that shall be born, that he hath done it.