< Zaburi 22 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
Unto the end. For the tasks of early morning. A Psalm of David. O God, my God, look upon me. Why have you forsaken me? Far from my salvation are the words of my offenses.
2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
My God, I will cry out by day, and you will not heed, and by night, and it will not be foolishness for me.
3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
But you dwell in holiness, O Praise of Israel.
4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
In you, our fathers have hoped. They hoped, and you freed them.
5 Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
They cried out to you, and they were saved. In you, they hoped and were not confounded.
6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
But I am a worm and not a man: a disgrace among men, and an outcast of the people.
7 Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
All those who saw me have derided me. They have spoken with the lips and shook the head.
8 Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
He has hoped in the Lord, let him rescue him. Let him save him because he chooses him.
9 Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
For you are the one who has drawn me out of the womb, my hope from the breasts of my mother.
10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
I have been thrown upon you from the womb; from the womb of my mother, you are my God.
11 Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
Do not depart from me. For tribulation is near, since there is no one who may help me.
12 Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
Many calves have surrounded me; fat bulls have besieged me.
13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
They have opened their mouths over me, just like a lion seizing and roaring.
14 Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
And so, I have been poured out like water, and all my bones have been scattered. My heart has become like wax, melting in the midst of my chest.
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
My strength has dried up like clay, and my tongue has adhered to my jaws. And you have pulled me down, into the dust of death.
16 Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
For many dogs have surrounded me. The council of the malicious has besieged me. They have pierced my hands and feet.
17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
They have numbered all my bones. And they have examined me and stared at me.
18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
They divided my garments among them, and over my vestment, they cast lots.
19 Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
But you, O Lord, do not take your help far from me; be attentive to my defense.
20 Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
O God, rescue my soul from the spear, and my only one from the hand of the dog.
21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
Save me from the mouth of the lion, and my humility from the horns of the single-horned beast.
22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
I will declare your name to my brothers. In the midst of the Church, I will praise you.
23 Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
You who fear the Lord, praise him. All the offspring of Jacob, glorify him.
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
May all the offspring of Israel fear him. For he has neither spurned nor despised the pleas of the poor. Neither has he turned his face away from me. And when I cried out to him, he heeded me.
25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
My praise is with you, within a great church. I will pay my vows in the sight of those who fear him.
26 Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
The poor will eat and be satisfied, and those who yearn for the Lord will praise him. Their hearts will live forever and ever.
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
All the ends of the earth will remember, and they will be converted to the Lord. And all the families of the Gentiles will adore in his sight.
28 kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
For the kingdom belongs to the Lord, and he will have dominion over the Gentiles.
29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
All the fat of the earth have gnashed their teeth, and they have adored. In his sight, they will fall down, all those who descend to the ground.
30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
And my soul will live for him, and my offspring will serve him.
31 Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.
There will be announced for the Lord a future generation, and the heavens will announce his justice to a people who will be born, whom the Lord has made.

< Zaburi 22 >