< Zaburi 22 >
1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
To the chief music-maker on Aijeleth-hash-shahar. A Psalm. Of David. My God, my God, why are you turned away from me? why are you so far from helping me, and from the words of my crying?
2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
O my God, I make my cry in the day, and you give no answer; and in the night, and have no rest.
3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
But you are holy, O you who are seated among the praises of Israel.
4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
Our fathers had faith in you: they had faith and you were their saviour.
5 Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
They sent up their cry to you and were made free: they put their faith in you and were not put to shame.
6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
But I am a worm and not a man; cursed by men, and looked down on by the people.
7 Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
I am laughed at by all those who see me: pushing out their lips and shaking their heads they say,
8 Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
He put his faith in the Lord; let the Lord be his saviour now: let the Lord be his saviour, because he had delight in him.
9 Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
But it was you who took care of me from the day of my birth: you gave me faith even from my mother's breasts.
10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
I was in your hands even before my birth; you are my God from the time when I was in my mother's body.
11 Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
Be not far from me, for trouble is near; there is no one to give help.
12 Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
A great herd of oxen is round me: I am shut in by the strong oxen of Bashan.
13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
I saw their mouths wide open, like lions crying after food.
14 Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
I am flowing away like water, and all my bones are out of place: my heart is like wax, it has become soft in my body.
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
My throat is dry like a broken vessel; my tongue is fixed to the roof of my mouth, and the dust of death is on my lips.
16 Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
Dogs have come round me: I am shut in by the band of evil-doers; they made wounds in my hands and feet.
17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
I am able to see all my bones; their looks are fixed on me:
18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
They make a division of my robes among them, by the decision of chance they take my clothing.
19 Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
Do not be far from me, O Lord: O my strength, come quickly to my help.
20 Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
Make my soul safe from the sword, my life from the power of the dog.
21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
Be my saviour from the lion's mouth; let me go free from the horns of the cruel oxen.
22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
I will give the knowledge of your name to my brothers: I will give you praise among the people.
23 Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
You who have fear of the Lord, give him praise; all you seed of Jacob, give him glory; go in fear of him, all you seed of Israel.
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
For he has not been unmoved by the pain of him who is troubled; or kept his face covered from him; but he has given an answer to his cry.
25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
My praise will be of you in the great meeting: I will make my offerings before his worshippers.
26 Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
The poor will have a feast of good things: those who make search for the Lord will give him praise: your heart will have life for ever.
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
All the ends of the earth will keep it in mind and be turned to the Lord: all the families of the nations will give him worship.
28 kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
For the kingdom is the Lord's; he is the ruler among the nations.
29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
All the fat ones of the earth will give him worship; all those who go down to the dust will make themselves low before him, even he who has not enough for the life of his soul.
30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
A seed will be his servant; the doings of the Lord will be made clear to the generation which comes after.
31 Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.
They will come and make his righteousness clear to a people of the future because he has done this.