< Zaburi 20 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Bwana na akujibu unapokuwa katika dhiki, jina la Mungu wa Yakobo na liwe kinga yako.
聖歌隊の指揮者によってうたわせたダビデの歌 主が悩みの日にあなたに答え、ヤコブの神のみ名があなたを守られるように。
2 Na akutumie msaada kutoka patakatifu na akupatie msaada kutoka Sayuni.
主が聖所から助けをあなたにおくり、シオンからあなたをささえ、
3 Na azikumbuke dhabihu zako zote, na azikubali sadaka zako za kuteketezwa.
あなたのもろもろの供え物をみ心にとめ、あなたの燔祭をうけられるように。 (セラ)
4 Na akujalie haja ya moyo wako, na aifanikishe mipango yako yote.
主があなたの心の願いをゆるし、あなたのはかりごとをことごとく遂げさせられるように。
5 Tutashangilia kwa furaha utakaposhinda, tutainua bendera zetu kwa jina la Mungu wetu. Bwana na akupe haja zako zote.
われらがあなたの勝利を喜びうたい、われらの神のみ名によって旗を揚げるように。主があなたの求めをすべて遂げさせられるように。
6 Sasa nafahamu kuwa Bwana humwokoa mpakwa mafuta wake, humjibu kutoka mbingu yake takatifu kwa nguvu za wokovu wa mkono wake wa kuume.
今わたしは知る、主はその油そそがれた者を助けられることを。主はその右の手による大いなる勝利をもってその聖なる天から彼に答えられるであろう。
7 Wengine wanatumaini magari ya vita, na wengine farasi, bali sisi tutalitumainia jina la Bwana, Mungu wetu.
ある者は戦車を誇り、ある者は馬を誇る。しかしわれらは、われらの神、主のみ名を誇る。
8 Wao wameshushwa chini na kuanguka, bali sisi tunainuka na kusimama imara.
彼らはかがみ、また倒れる。しかしわれらは起きて、まっすぐに立つ。
9 Ee Bwana, mwokoe mfalme! Tujibu tunapokuita!
主よ、王に勝利をおさずけください。われらが呼ばわる時、われらにお答えください。

< Zaburi 20 >