< Zaburi 2 >

1 Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
¿Por qué se amotinan las gentes, y los pueblos piensan vanidad?
2 Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
Estarán los reyes de la tierra, y príncipes consultarán en uno contra Jehová, y contra su ungido, diciendo:
3 Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
Rompamos sus coyundas: y echemos de nosotros sus cuerdas.
4 Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
El que mora en los cielos se reirá: el Señor se burlará de ellos.
5 Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
Entonces hablará a ellos con su furor, y con su ira los conturbará.
6 “Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
Y yo te establecí mi rey sobre Sión, el monte de mi santidad.
7 Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
Yo recitaré el decreto. Jehová me dijo: Mi hijo eres tú: yo te engendré hoy.
8 Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
Demándame, y yo daré las gentes por tu heredad, y por tu posesión los cabos de la tierra.
9 Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
Quebrantarlos has con vara de hierro: como vaso de ollero los desmenuzarás.
10 Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
Y ahora reyes entendéd: admitid consejo jueces de la tierra.
11 Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
Servíd a Jehová con temor: y alegráos con temblor.
12 Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.
Besád al hijo, porque no se enoje, y perezcáis en el camino: cuando se encendiere un poco su furor, bienaventurados todos los que confían en él.

< Zaburi 2 >