< Zaburi 2 >

1 Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
Por que as nações se rebelam, e os povos planejam em vão?
2 Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
Os reis da terra se levantam, e os governantes tomam conselhos reunidos contra o SENHOR, e contra seu Ungido, [dizendo]:
3 Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
Rompamos as correntes deles, e lancemos fora de nós as cordas deles.
4 Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
Aquele que está sentado nos céus rirá; o Senhor zombará deles.
5 Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
Então ele lhes falará em sua ira; em seu furor ele os assombrará, [dizendo]:
6 “Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
E eu ungi a meu Rei sobre Sião, o monte de minha santidade.
7 Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
E eu declararei o decreto do SENHOR: Ele me disse: Tu és meu Filho; eu hoje te gerei.
8 Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
Pede-me, e eu te darei as nações [por] herança, e [por] tua propriedade os confins da terra.
9 Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
Com cetro de ferro tu as quebrarás; como vaso de oleiro tu as despedaçarás;
10 Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
Portanto agora, reis, sede prudentes; vós, juízes da terra, deixai serdes instruídos.
11 Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
Servi ao SENHOR com temor; e alegrai-vos com tremor.
12 Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.
Beijai ao Filho, para que ele não se ire, e pereçais [no] caminho; porque em breve a ira dele se acenderá. Bem-aventurados [são] todos os que nele confiam.

< Zaburi 2 >