< Zaburi 2 >

1 Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
Warum toben die Heiden und reden die Völker vergeblich?
2 Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
Die Könige der Erde stehen zusammen, und die Fürsten verabreden sich wider den HERRN und wider seinen Gesalbten:
3 Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
«Wir wollen ihre Bande zerreißen und ihre Fesseln von uns werfen!»
4 Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
Der im Himmel thront, lacht, der HERR spottet ihrer.
5 Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
Dann wird er zu ihnen reden in seinem Zorn und sie schrecken mit seinem Grimm:
6 “Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
«Ich habe meinen König eingesetzt auf Zion, meinem heiligen Berge!»
7 Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
Ich will erzählen vom Ratschluß des HERRN; er hat zu mir gesagt: «Du bist mein Sohn, heute habe ich dich gezeugt
8 Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
Heische von mir, so will ich dir die Nationen zum Erbe geben und die Enden der Erde zu deinem Eigentum.
9 Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
Du sollst sie mit eisernem Zepter zerschmettern, wie Töpfergeschirr sie zerschmeißen!»
10 Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
So nehmet nun Verstand an, ihr Könige, und lasset euch warnen, ihr Richter der Erde!
11 Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
Dienet dem HERRN mit Furcht und frohlocket mit Zittern.
12 Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.
Küsset den Sohn, daß er nicht zürne und ihr nicht umkommet auf dem Wege; denn wie leicht kann sein Zorn entbrennen! Wohl allen, die sich bergen bei ihm!

< Zaburi 2 >