< Zaburi 2 >
1 Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
Was soll das Toben der Völker und das eitle Sinnen der Völkerschaften?
2 Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
Die Könige der Erde rotten sich zusammen, und die Fürsten halten Rat miteinander gegen den HERRN und den von ihm Gesalbten:
3 Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
»Laßt uns zerreißen ihre Bande und von uns werfen ihre Fesseln!«
4 Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
Der im Himmel thront, der lacht, der Allherr spottet ihrer.
5 Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
Dann aber wird er zu ihnen reden in seinem Zorn und sie schrecken in seinem Ingrimm:
6 “Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
»Habe ich doch meinen König eingesetzt auf dem Zion, meinem heiligen Berge!« –
7 Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
Laßt mich kundtun den Ratschluß des HERRN! Er hat zu mir gesagt: »Mein Sohn bist du; ich selbst habe heute dich gezeugt.
8 Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
Fordre von mir, so gebe ich dir die Völker zum Erbe und dir zum Besitz die Enden der Erde.
9 Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
Du sollst sie mit eiserner Keule zerschmettern, wie Töpfergeschirr sie zerschlagen!« –
10 Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
So nehmt denn Klugheit an, ihr Könige, laßt euch warnen, ihr Richter der Erde!
11 Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
Dienet dem HERRN mit Furcht und jubelt ihm zu mit Zittern!
12 Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.
Küsset den Sohn, auf daß er nicht zürne und ihr zugrunde geht auf eurem Wege! denn leicht entbrennt sein Zorn. Wohl allen, die bei ihm sich bergen!