< Zaburi 2 >

1 Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
Pourquoi les nations ont-elles. frémi, et les peuples médité des choses vaines?
2 Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
Les rois de la terre se sont levés, et les princes se sont ligués contre le Seigneur et contre son Christ.
3 Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
Rompons leurs liens, ont-ils dit, et rejetons loin de nous leur joug.
4 Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
Celui qui habite dans les cieux se rira d’eux, et le Seigneur se moquera d’eux.
5 Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
Alors il leur parlera dans sa colère, et dans sa fureur il les confondra.
6 “Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
Pour moi, j’ai été établi roi par lui sur Sion, sa montagne sainte, annonçant ses préceptes.
7 Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
Le Seigneur m’a dit: Vous êtes mon Fils, c’est moi qui aujourd’hui vous ai engendré.
8 Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
Demandez-moi, et je vous donnerai les nations en héritage, et en possession les extrémités de la terre.
9 Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
Vous les gouvernerez avec une verge de fer, et vous les briserez comme un vase de potier.
10 Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
Et maintenant, ô rois, comprenez; instruisez-vous, vous qui jugez la terre.
11 Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
Servez le Seigneur dans la crainte, et réjouissez-vous en lui avec tremblement.
12 Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.
Embrassez la doctrine, de peur que quelque jour le Seigneur ne s’irrite, et que vous ne périssiez hors de la voie de la justice. Lorsque sa colère s’enflammera en un instant, heureux tous ceux qui se confient en lui.

< Zaburi 2 >