< Zaburi 2 >
1 Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
Pourquoi les nations s'agitent-elles? Pourquoi les peuples forment-ils de vains projets?
2 Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
Les rois de la terre se sont soulevés, Et les princes conspirent ensemble Contre l'Éternel et contre son Oint.
3 Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
— Rompons leurs liens, disent-ils. Et jetons loin de nous leurs chaînes!
4 Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
— Celui qui habite dans les deux en rira; Le Seigneur se moquera d'eux.
5 Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
Alors il leur parlera dans sa colère; Il les épouvantera par son courroux.
6 “Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
— Et moi, dira-t-il, j'ai sacré mon roi Sur Sion, ma montagne sainte.
7 Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
— Je publierai le décret. L'Éternel m'a dit: «Tu es mon Fils; Aujourd'hui je t'ai engendré.
8 Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
Demande-moi, et je te donnerai pour héritage les nations. Pour possession les extrémités de la terre.
9 Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
Tu les briseras avec un sceptre de fer; Tu les mettras en pièces comme un vase de potier.»
10 Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
Maintenant donc, ô rois, ayez de l'intelligence; Laissez-vous instruire, juges de la terre!
11 Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
Servez l'Éternel avec crainte. Et réjouissez-vous avec tremblement.
12 Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.
Rendez hommage au Fils, de peur qu'il ne s'irrite, Et que vous ne périssiez dans la voie que vous suivez; Car sa colère est prompte à s'enflammer. Heureux tous ceux qui cherchent leur refuge en lui!