< Zaburi 2 >

1 Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
Pourquoi s’agitent les nations, et les peuples méditent-ils la vanité?
2 Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
Les rois de la terre se lèvent, et les princes consultent ensemble contre l’Éternel et contre son Oint:
3 Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
Rompons leurs liens, et jetons loin de nous leurs cordes!
4 Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
Celui qui habite dans les cieux se rira [d’eux], le Seigneur s’en moquera.
5 Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
Alors il leur parlera dans sa colère, et, dans sa fureur, il les épouvantera:
6 “Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
Et moi, j’ai oint mon roi sur Sion, la montagne de ma sainteté.
7 Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
Je raconterai le décret: l’Éternel m’a dit: Tu es mon Fils; aujourd’hui, je t’ai engendré.
8 Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
Demande-moi, et je te donnerai les nations pour héritage, et, pour ta possession, les bouts de la terre;
9 Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
Tu les briseras avec un sceptre de fer; comme un vase de potier tu les mettras en pièces.
10 Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
Et maintenant, ô rois, soyez intelligents; vous, juges de la terre, recevez instruction:
11 Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
Servez l’Éternel avec crainte, et réjouissez-vous avec tremblement;
12 Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.
Embrassez le Fils, de peur qu’il ne s’irrite, et que vous ne périssiez dans le chemin, quand sa colère s’embrasera tant soit peu. Bienheureux tous ceux qui se confient en lui!

< Zaburi 2 >