< Zaburi 2 >
1 Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
Pourquoi les nations se déchaînent-elles? et les peuples complotent en vain?
2 Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
Les rois de la terre prennent position, et les dirigeants se concertent, contre Yahvé et contre son oint, en disant,
3 Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
« Brisons leurs liens, et jette leurs cordes loin de nous. »
4 Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
Celui qui est assis dans les cieux rira. Le Seigneur les tournera en dérision.
5 Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
Puis il leur parlera dans sa colère, et les terrifier dans sa colère:
6 “Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
« Mais j'ai établi mon roi sur ma sainte colline de Sion. »
7 Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
Je vais raconter le décret: Yahvé m'a dit: « Tu es mon fils. Aujourd'hui, je suis devenu votre père.
8 Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
Demande-moi, et je te donnerai les nations en héritage, les extrémités de la terre pour les posséder.
9 Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
Tu les briseras avec une verge de fer. Tu les briseras comme le vase d'un potier. »
10 Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
Maintenant, soyez sages, vous les rois. Soyez instruits, juges de la terre.
11 Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
Servez Yahvé avec crainte, et se réjouir en tremblant.
12 Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.
Rendez un hommage sincère au Fils, de peur qu'il ne se mette en colère et que vous ne périssiez en chemin, car sa colère va bientôt s'enflammer. Heureux tous ceux qui se réfugient en lui.