< Zaburi 2 >
1 Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
Why have nations tumultuously assembled? And do peoples meditate vanity?
2 Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
Station themselves do kings of the earth, And princes have been united together, Against Jehovah, and against His Messiah:
3 Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
'Let us draw off Their cords, And cast from us Their thick bands.'
4 Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
He who is sitting in the heavens doth laugh, The Lord doth mock at them.
5 Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
Then doth He speak unto them in His anger, And in His wrath He doth trouble them:
6 “Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
'And I — I have anointed My King, Upon Zion — My holy hill.'
7 Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
I declare concerning a statute: Jehovah said unto me, 'My Son Thou [art], I to-day have brought thee forth.
8 Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
Ask of Me and I give nations — thy inheritance, And thy possession — the ends of earth.
9 Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
Thou dost rule them with a sceptre of iron, As a vessel of a potter Thou dost crush them.'
10 Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
And now, O kings, act wisely, Be instructed, O judges of earth,
11 Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
Serve ye Jehovah with fear, And rejoice with trembling.
12 Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.
Kiss the Chosen One, lest He be angry, And ye lose the way, When His anger burneth but a little, O the happiness of all trusting in Him!