< Zaburi 2 >

1 Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
Whi gnastiden with teeth hethene men; and puplis thouyten veyn thingis?
2 Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
The kyngis of erthe stoden togidere; and princes camen togidere ayens the Lord, and ayens his Crist?
3 Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
Breke we the bondis of hem; and cast we awei the yok of hem fro vs.
4 Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
He that dwellith in heuenes schal scorne hem; and the Lord schal bimowe hem.
5 Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
Thanne he schal speke to hem in his ire; and he schal disturble hem in his stronge veniaunce.
6 “Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
Forsothe Y am maad of hym a kyng on Syon, his hooli hil; prechynge his comaundement.
7 Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
The Lord seide to me, Thou art my sone; Y haue gendrid thee to dai.
8 Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
Axe thou of me, and Y schal yyue to thee hethene men thin eritage; and thi possessioun the termes of erthe.
9 Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
Thou schalt gouerne hem in an yrun yerde; and thou schalt breke hem as the vessel of a pottere.
10 Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
And now, ye kyngis, vndurstonde; ye that demen the erthe, be lerud.
11 Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
Serue ye the Lord with drede; and make ye ful ioye to hym with tremblyng.
12 Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.
Take ye lore; lest the Lord be wrooth sumtyme, and lest ye perischen fro iust waie. Whanne his `ire brenneth out in schort tyme; blessed ben alle thei, that tristen in hym.

< Zaburi 2 >