< Zaburi 2 >
1 Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
to/for what? to throng nation and people to mutter vain
2 Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
to stand king land: country/planet and to rule to found unitedness upon LORD and upon anointed his
3 Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
to tear [obj] bond their and to throw from us cord their
4 Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
to dwell in/on/with heaven to laugh Lord to mock to/for them
5 Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
then to speak: speak to(wards) them in/on/with face: anger his and in/on/with burning anger his to dismay them
6 “Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
and I to install king my upon Zion mountain: mount holiness my
7 Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
to recount to(wards) statute: decree LORD to say to(wards) me son: child my you(m. s.) I [the] day to beget you
8 Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
to ask from me and to give: make nation inheritance your and possession your end land: country/planet
9 Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
to shatter them in/on/with tribe: staff iron like/as article/utensil to form: potter to shatter them
10 Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
and now king be prudent to discipline to judge land: country/planet
11 Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
to serve: minister [obj] LORD in/on/with fear and to rejoice in/on/with trembling
12 Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.
to kiss son: child lest be angry and to perish way: journey for to burn: burn like/as little face: anger his blessed all to seek refuge in/on/with him