< Zaburi 2 >
1 Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
Wherefore did the heathen rage, and the nations imagine vain things?
2 Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
The kings of the earth stood up, and the rulers gathered themselves together, against the Lord, and against his Christ;
3 Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
[saying], Let us break through their bonds, and cast away their yoke from us.
4 Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
He that dwells in the heavens shall laugh them to scorn, and the Lord shall mock them.
5 Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
Then shall he speak to them in his anger, and trouble them in his fury.
6 “Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
But I have been made king by him on Sion his holy mountain,
7 Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
declaring the ordinance of the Lord: the Lord said to me, Thou art my Son, to-day have I begotten thee.
8 Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
Ask of me, and I will give thee the heathen [for] thine inheritance, and the ends of the earth [for] thy possession.
9 Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
Thou shalt rule them with a rod of iron; thou shalt dash them in pieces as a potter's vessel.
10 Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
Now therefore understand, ye kings: be instructed, all ye that judge the earth.
11 Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
Serve the Lord with fear, and rejoice in him with trembling.
12 Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.
Accept correction, lest at any time the Lord be angry, and ye should perish from the righteous way: whensoever his wrath shall be suddenly kindled, blessed are all they that trust in him.