< Zaburi 2 >
1 Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
外邦为什么争闹? 万民为什么谋算虚妄的事?
2 Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
世上的君王一齐起来, 臣宰一同商议, 要敌挡耶和华并他的受膏者,
3 Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
说:我们要挣开他们的捆绑, 脱去他们的绳索。
4 Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
那坐在天上的必发笑; 主必嗤笑他们。
5 Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
那时,他要在怒中责备他们, 在烈怒中惊吓他们,
6 “Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
说:我已经立我的君 在锡安—我的圣山上了。
7 Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
受膏者说:我要传圣旨。 耶和华曾对我说:你是我的儿子, 我今日生你。
8 Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
你求我,我就将列国赐你为基业, 将地极赐你为田产。
9 Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
你必用铁杖打破他们; 你必将他们如同窑匠的瓦器摔碎。
10 Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
现在,你们君王应当省悟! 你们世上的审判官该受管教!
11 Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
当存畏惧事奉耶和华, 又当存战兢而快乐。
12 Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.
当以嘴亲子,恐怕他发怒, 你们便在道中灭亡, 因为他的怒气快要发作。 凡投靠他的,都是有福的。