< Zaburi 19 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, anga zahubiri kazi ya mikono yake.
Jusqu'à la Fin, psaume de David. Les cieux racontent la gloire du Seigneur, et le firmament fait connaître l'œuvre de ses mains.
2 Siku baada ya siku zinatoa habari, usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
Le jour parle de lui au jour; la nuit montre sa science à la nuit.
3 Hakuna msemo wala lugha, ambapo sauti zao hazisikiki.
Il n'y a langage ni paroles dont leur voix ne soit entendue.
4 Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu. Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
Leur voix s'est répandue sur toute la terre; leur parole est parvenue au bout du monde. Il a tendu son tabernacle dans le soleil;
5 linafanana na bwana arusi akitoka chumbani mwake, kama shujaa afurahiavyo kukamilisha kushindana kwake.
Et le soleil ressemble au jeune époux sortant de son lit nuptial, il a tressailli de joie comme un géant pour courir dans sa voie.
6 Huchomoza upande mmoja wa mbingu, na kufanya mzunguko wake hadi upande mwingine. Hakuna kilichojificha joto lake.
Il sort de l'extrémité du ciel; et son issue est à l'autre extrémité; et nul ne peut se mettre à l'abri de sa chaleur.
7 Sheria ya Bwana ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za Bwana ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.
La loi du Seigneur est immaculée, elle convertit les âmes; le témoignage du Seigneur est fidèle, il donne la sagesse aux enfants.
8 Maagizo ya Bwana ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za Bwana huangaza, zatia nuru machoni.
La justice du Seigneur est droite, elle réjouit le cœur; les préceptes du Seigneur brillent d'un vif éclat, ils éclairent les yeux.
9 Kumcha Bwana ni utakatifu, nako kwadumu milele. Amri za Bwana ni za hakika, nazo zina haki.
La crainte du Seigneur est sainte, elle persiste dans les siècles des siècles; les jugements du Seigneur sont vrais, et justifiés en eux-mêmes.
10 Ni za thamani kuliko dhahabu, kuliko dhahabu iliyo safi sana, ni tamu kuliko asali, kuliko asali kutoka kwenye sega.
Ils sont infiniment plus désirables que l'or et les pierres précieuses; ils sont plus doux que le miel et que les rayons de miel.
11 Kwa hizo mtumishi wako anaonywa, katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
Aussi ton serviteur les garde-t-il; à les garder on gagne un riche salaire.
12 Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
Qui a conscience de ses chutes? Purifies-moi de mes fautes les plus cachées.
13 Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi, nazo zisinitawale. Ndipo nitakapokuwa sina lawama, wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.
Préserve ton serviteur des vices des étrangers. S'ils ne me dominent pas, alors je serai sans souillure et lavé d'un grand péché.
14 Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu, yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu na Mkombozi wangu.
Alors les paroles de ma bouche te plairont, et les pensées de mon cœur seront toujours agréables devant toi. Seigneur, tu es mon aide et mon Rédempteur.

< Zaburi 19 >