< Zaburi 19 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, anga zahubiri kazi ya mikono yake.
To victorie, the salm of Dauid. Heuenes tellen out the glorie of God; and the firmament tellith the werkis of hise hondis.
2 Siku baada ya siku zinatoa habari, usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
The dai tellith out to the dai a word; and the nyyt schewith kunnyng to the nyyt.
3 Hakuna msemo wala lugha, ambapo sauti zao hazisikiki.
No langagis ben, nether wordis; of whiche the voices of hem ben not herd.
4 Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu. Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
The soun of hem yede out in to al erthe; and the wordis of hem `yeden out in to the endis of the world.
5 linafanana na bwana arusi akitoka chumbani mwake, kama shujaa afurahiavyo kukamilisha kushindana kwake.
In the sunne he hath set his tabernacle; and he as a spouse comynge forth of his chaumbre. He fulli ioyede, as a giaunt, to renne his weie;
6 Huchomoza upande mmoja wa mbingu, na kufanya mzunguko wake hadi upande mwingine. Hakuna kilichojificha joto lake.
his goynge out was fro hiyeste heuene. And his goyng ayen was to the hiyeste therof; and noon is that hidith hym silf fro his heet.
7 Sheria ya Bwana ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za Bwana ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.
The lawe of the Lord is with out wem, and conuertith soulis; the witnessyng of the Lord is feithful, and yyueth wisdom to litle children.
8 Maagizo ya Bwana ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za Bwana huangaza, zatia nuru machoni.
The riytfulnessis of the Lord ben riytful, gladdynge hertis; the comaundement of the Lord is cleere, liytnynge iyen.
9 Kumcha Bwana ni utakatifu, nako kwadumu milele. Amri za Bwana ni za hakika, nazo zina haki.
The hooli drede of the Lord dwellith in to world of world; the domes of the Lord ben trewe, iustified in to hem silf.
10 Ni za thamani kuliko dhahabu, kuliko dhahabu iliyo safi sana, ni tamu kuliko asali, kuliko asali kutoka kwenye sega.
Desirable more than gold, and a stoon myche preciouse; and swettere than hony and honycoomb.
11 Kwa hizo mtumishi wako anaonywa, katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
`Forwhi thi seruaunt kepith thoo; myche yeldyng is in tho to be kept.
12 Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
Who vndurstondith trespassis? make thou me cleene fro my priuy synnes;
13 Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi, nazo zisinitawale. Ndipo nitakapokuwa sina lawama, wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.
and of alien synnes spare thi seruaunt. `If the forseid defautis ben not, Lord, of me, than Y schal be with out wem; and Y schal be clensid of the mooste synne.
14 Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu, yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu na Mkombozi wangu.
And the spechis of my mouth schulen be, that tho plese; and the thenkynge of myn herte euere in thi siyt. Lord, myn helpere; and myn ayenbiere.

< Zaburi 19 >