< Zaburi 19 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, anga zahubiri kazi ya mikono yake.
[When people look at everything that] God [has placed in] the skies, they can see that he is very great; they can see the great things that he has created.
2 Siku baada ya siku zinatoa habari, usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
Day after day [it is as though the sun] proclaims [the glory of God], and night after night [it is as though the moon and stars] say that they know [that God made them].
3 Hakuna msemo wala lugha, ambapo sauti zao hazisikiki.
They do not really speak; they do not say any words. There is no voice [from them] for anyone to hear.
4 Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu. Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
But what they declare [about God] goes throughout the world, and [even people who live in] the most distant/remote places on earth can know it. The sun is in the skies where God placed it [MET];
5 linafanana na bwana arusi akitoka chumbani mwake, kama shujaa afurahiavyo kukamilisha kushindana kwake.
it rises each morning like a bridegroom [who is happy] as he comes out of his bedroom after his wedding. It is like a strong athlete who is very eager to start running in a race.
6 Huchomoza upande mmoja wa mbingu, na kufanya mzunguko wake hadi upande mwingine. Hakuna kilichojificha joto lake.
The sun rises at one side of the sky and goes across [the sky and sets on] the other side, and nothing can hide from its heat.
7 Sheria ya Bwana ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za Bwana ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.
The instructions that Yahweh has given us are perfect; they (revive us/give us new strength). We can be sure that the things that Yahweh has told us will never change, and [by learning them] people who have not been previously taught/instructed will become wise.
8 Maagizo ya Bwana ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za Bwana huangaza, zatia nuru machoni.
Yahweh’s laws are fair/just; [when we obey them], we become joyful. The commands of Yahweh are clear, and [by reading them] [PRS] we start to understand [how God wants us to behave].
9 Kumcha Bwana ni utakatifu, nako kwadumu milele. Amri za Bwana ni za hakika, nazo zina haki.
It is good for people to revere Yahweh; that is something that they will do forever. What Yahweh has decided is fair, and it is always right.
10 Ni za thamani kuliko dhahabu, kuliko dhahabu iliyo safi sana, ni tamu kuliko asali, kuliko asali kutoka kwenye sega.
The things that God has decided are more valuable than gold, even the finest/purest gold. They are sweeter than honey that drips from honeycombs.
11 Kwa hizo mtumishi wako anaonywa, katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
Furthermore, [by reading them] I learn [what things are good to do and what things are evil], and they promise a great reward to [us who] obey them.
12 Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
But there is no one who can know all his errors [RHQ]; so Yahweh, forgive me for these things which I do that I do not realize are wrong.
13 Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi, nazo zisinitawale. Ndipo nitakapokuwa sina lawama, wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.
Keep me from doing things that I know are wrong; do not let my sinful desires control me. If you do that, I will no longer be guilty for committing such sins, and I will not commit the great sin [of rebelling terribly] against you.
14 Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu, yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu na Mkombozi wangu.
O Yahweh, you are [like] an [overhanging] rock [MET] under which I can be safe; you are the one who protects me. I hope/desire that the things that I say and what I think will [always] please you.

< Zaburi 19 >