< Zaburi 19 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, anga zahubiri kazi ya mikono yake.
For the leader. A psalm of David. The heavens declare God’s glory, the sky tells what his hands have done.
2 Siku baada ya siku zinatoa habari, usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
Day tells it to day, night reveals it to night,
3 Hakuna msemo wala lugha, ambapo sauti zao hazisikiki.
without speaking, without words; without the sound of voices.
4 Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu. Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
But through all the world their voice carries their words to the ends of the earth. He has pitched a tent for the sun in the sky,
5 linafanana na bwana arusi akitoka chumbani mwake, kama shujaa afurahiavyo kukamilisha kushindana kwake.
it comes out like a bridegroom from his bridal chamber, it joyfully runs its course like a hero.
6 Huchomoza upande mmoja wa mbingu, na kufanya mzunguko wake hadi upande mwingine. Hakuna kilichojificha joto lake.
From one end of the heavens it rises, and around it runs to the other, and nothing hides from its heat.
7 Sheria ya Bwana ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za Bwana ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.
The law of the Lord is perfect, renewing life. The decrees of the Lord are trusty, making the simple wise.
8 Maagizo ya Bwana ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za Bwana huangaza, zatia nuru machoni.
The behests of the Lord are right, rejoicing the heart. The command of the Lord is pure, giving light to the eyes.
9 Kumcha Bwana ni utakatifu, nako kwadumu milele. Amri za Bwana ni za hakika, nazo zina haki.
The fear of the Lord is clean, it endures forever. The Lord’s judgments are true and right altogether.
10 Ni za thamani kuliko dhahabu, kuliko dhahabu iliyo safi sana, ni tamu kuliko asali, kuliko asali kutoka kwenye sega.
More precious are they than gold – than fine gold in plenty, and sweeter they are than honey, that drops from the comb.
11 Kwa hizo mtumishi wako anaonywa, katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
By them is your servant warned; who keeps them has rich reward.
12 Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
Who can know their flaws? Absolve me from those I know not.
13 Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi, nazo zisinitawale. Ndipo nitakapokuwa sina lawama, wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.
Keep your servant from wilful sins – from falling under their sway: then blameless and clear will I be from great offense.
14 Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu, yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu na Mkombozi wangu.
May the words of my mouth and the thoughts of my heart be pleasing to you, Lord, my rock and redeemer.