< Zaburi 19 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, anga zahubiri kazi ya mikono yake.
“For the leader of the music. A psalm of David.” The heavens declare the glory of God; The firmament showeth forth the work of his hands.
2 Siku baada ya siku zinatoa habari, usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
Day uttereth instruction unto day, And night showeth knowledge unto night.
3 Hakuna msemo wala lugha, ambapo sauti zao hazisikiki.
They have no speech nor language, And their voice is not heard;
4 Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu. Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
Yet their sound goeth forth to all the earth, And their words to the ends of the world. In them hath he set a tabernacle for the sun,
5 linafanana na bwana arusi akitoka chumbani mwake, kama shujaa afurahiavyo kukamilisha kushindana kwake.
Which cometh forth like a bridegroom from his chamber, And rejoiceth, like a strong man, to run his course.
6 Huchomoza upande mmoja wa mbingu, na kufanya mzunguko wake hadi upande mwingine. Hakuna kilichojificha joto lake.
He goeth forth from the extremity of heaven, And maketh his circuit to the end of it; And nothing is hid from his heat.
7 Sheria ya Bwana ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za Bwana ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.
The law of the LORD is perfect, reviving the soul; The precepts of the LORD are sure, making wise the simple;
8 Maagizo ya Bwana ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za Bwana huangaza, zatia nuru machoni.
The statutes of the LORD are right, rejoicing the heart; The commandments of the LORD are pure, enlightening the eyes;
9 Kumcha Bwana ni utakatifu, nako kwadumu milele. Amri za Bwana ni za hakika, nazo zina haki.
The fear of the LORD is clean, enduring for ever; The judgments of the LORD are true and righteous altogether.
10 Ni za thamani kuliko dhahabu, kuliko dhahabu iliyo safi sana, ni tamu kuliko asali, kuliko asali kutoka kwenye sega.
More precious are they than gold; yea, than much fine gold; Sweeter than honey and the honeycomb.
11 Kwa hizo mtumishi wako anaonywa, katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
By them also is thy servant warned, And in keeping of them there is great reward.
12 Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
Who knoweth his own offences? Oh, cleanse thou me from secret faults!
13 Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi, nazo zisinitawale. Ndipo nitakapokuwa sina lawama, wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.
Keep back also thy servant from presumptuous sins; Let them not have dominion over me! Then shall I be upright; I shall not be polluted with gross transgression.
14 Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu, yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu na Mkombozi wangu.
May the words of my mouth and the meditation of my heart Be acceptable in thy sight, O LORD, my strength and my redeemer!