< Zaburi 19 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, anga zahubiri kazi ya mikono yake.
For the Leader. A Psalm of David. The heavens declare the glory of God, and the firmament showeth His handiwork;
2 Siku baada ya siku zinatoa habari, usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
Day unto day uttereth speech, and night unto night revealeth knowledge;
3 Hakuna msemo wala lugha, ambapo sauti zao hazisikiki.
There is no speech, there are no words, neither is their voice heard.
4 Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu. Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
Their line is gone out through all the earth, and their words to the end of the world. In them hath He set a tent for the sun,
5 linafanana na bwana arusi akitoka chumbani mwake, kama shujaa afurahiavyo kukamilisha kushindana kwake.
Which is as a bridegroom coming out of his chamber, and rejoiceth as a strong man to run his course.
6 Huchomoza upande mmoja wa mbingu, na kufanya mzunguko wake hadi upande mwingine. Hakuna kilichojificha joto lake.
His going forth is from the end of the heaven, and his circuit unto the ends of it; and there is nothing hid from the heat thereof.
7 Sheria ya Bwana ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za Bwana ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.
The law of the LORD is perfect, restoring the soul; the testimony of the LORD is sure, making wise the simple.
8 Maagizo ya Bwana ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za Bwana huangaza, zatia nuru machoni.
The precepts of the LORD are right, rejoicing the heart; the commandment of the LORD is pure, enlightening the eyes.
9 Kumcha Bwana ni utakatifu, nako kwadumu milele. Amri za Bwana ni za hakika, nazo zina haki.
The fear of the LORD is clean, enduring for ever; the ordinances of the LORD are true, they are righteous altogether;
10 Ni za thamani kuliko dhahabu, kuliko dhahabu iliyo safi sana, ni tamu kuliko asali, kuliko asali kutoka kwenye sega.
More to be desired are they than gold, yea, than much fine gold; sweeter also than honey and the honeycomb.
11 Kwa hizo mtumishi wako anaonywa, katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
Moreover by them is Thy servant warned; in keeping of them there is great reward.
12 Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
Who can discern his errors? Clear Thou me from hidden faults.
13 Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi, nazo zisinitawale. Ndipo nitakapokuwa sina lawama, wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.
Keep back Thy servant also from presumptuous sins, that they may not have dominion over me; then shall I be faultless, and I shall be clear from great transgression.
14 Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu, yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu na Mkombozi wangu.
Let the words of my mouth and the meditation of my heart be acceptable before Thee, O LORD, my Rock, and my Redeemer.

< Zaburi 19 >