< Zaburi 19 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, anga zahubiri kazi ya mikono yake.
To him that excelleth. A Psalme of Dauid. The heauens declare the glory of God, and the firmament sheweth ye worke of his hands.
2 Siku baada ya siku zinatoa habari, usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
Day vnto day vttereth the same, and night vnto night teacheth knowledge.
3 Hakuna msemo wala lugha, ambapo sauti zao hazisikiki.
There is no speach nor language, where their voyce is not heard.
4 Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu. Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
Their line is gone forth through all the earth, and their words into the endes of the world: in them hath he set a tabernacle for the sunne.
5 linafanana na bwana arusi akitoka chumbani mwake, kama shujaa afurahiavyo kukamilisha kushindana kwake.
Which commeth forth as a bridegrome out of his chamber, and reioyceth like a mightie man to runne his race.
6 Huchomoza upande mmoja wa mbingu, na kufanya mzunguko wake hadi upande mwingine. Hakuna kilichojificha joto lake.
His going out is from the ende of the heauen, and his compasse is vnto the endes of ye same, and none is hid from the heate thereof.
7 Sheria ya Bwana ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za Bwana ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.
The Lawe of the Lord is perfite, conuerting the soule: the testimonie of the Lord is sure, and giueth wisedome vnto the simple.
8 Maagizo ya Bwana ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za Bwana huangaza, zatia nuru machoni.
The statutes of the Lord are right and reioyce the heart: the commandement of the Lord is pure, and giueth light vnto the eyes.
9 Kumcha Bwana ni utakatifu, nako kwadumu milele. Amri za Bwana ni za hakika, nazo zina haki.
The feare of the Lord is cleane, and indureth for euer: the iudgements of the Lord are trueth: they are righteous altogether,
10 Ni za thamani kuliko dhahabu, kuliko dhahabu iliyo safi sana, ni tamu kuliko asali, kuliko asali kutoka kwenye sega.
And more to be desired then golde, yea, then much fine golde: sweeter also then honie and the honie combe.
11 Kwa hizo mtumishi wako anaonywa, katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
Moreouer by them is thy seruant made circumspect, and in keeping of them there is great reward.
12 Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
Who can vnderstand his faultes? clense me from secret fautes.
13 Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi, nazo zisinitawale. Ndipo nitakapokuwa sina lawama, wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.
Keepe thy seruant also from presumptuous sinnes: let them not reigne ouer me: so shall I be vpright, and made cleane from much wickednes.
14 Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu, yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu na Mkombozi wangu.
Let the wordes of my mouth, and the meditation of mine heart be acceptable in thy sight, O Lord, my strength, and my redeemer.

< Zaburi 19 >