< Zaburi 19 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, anga zahubiri kazi ya mikono yake.
For the music director. A psalm of David. The heavens declare God's glory; the skies above announce what he has made.
2 Siku baada ya siku zinatoa habari, usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
Each day speaks constantly about God's glory to the next day; each night shares knowledge of God with the next night.
3 Hakuna msemo wala lugha, ambapo sauti zao hazisikiki.
They speak without speech or words; their voice is not audible;
4 Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu. Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
Yet what they say is heard all over the earth; their message goes to the whole world. God has made a home in the heavens for the sun.
5 linafanana na bwana arusi akitoka chumbani mwake, kama shujaa afurahiavyo kukamilisha kushindana kwake.
It's like a bridegroom coming out of his room, like a fit athlete happy to run a race.
6 Huchomoza upande mmoja wa mbingu, na kufanya mzunguko wake hadi upande mwingine. Hakuna kilichojificha joto lake.
It rises on one side of the heavens and travels across to the other. Nothing is hidden from its heat.
7 Sheria ya Bwana ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za Bwana ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.
The Lord's law is beneficial, renewing spiritual life. The Lord's teaching is trustworthy, making inexperienced people wise.
8 Maagizo ya Bwana ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za Bwana huangaza, zatia nuru machoni.
The Lord's instructions are right, making people glad. The Lord's commandments are sincere, helping people see what is good.
9 Kumcha Bwana ni utakatifu, nako kwadumu milele. Amri za Bwana ni za hakika, nazo zina haki.
Reverence for the Lord is right, and lasts forever. The Lord's judgments are both true and fair.
10 Ni za thamani kuliko dhahabu, kuliko dhahabu iliyo safi sana, ni tamu kuliko asali, kuliko asali kutoka kwenye sega.
They are more to be valued than gold, even the finest gold; they are sweeter than honey, even the purest honey coming straight from the honeycomb.
11 Kwa hizo mtumishi wako anaonywa, katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
They also warn your servant. By keeping them I'm richly rewarded.
12 Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
Who's aware of their own mistakes? Don't punish me for these faults I'm unaware of.
13 Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi, nazo zisinitawale. Ndipo nitakapokuwa sina lawama, wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.
Don't let your servant commit deliberate sins. Don't let them rule over me. Then I will be without fault, innocent of such rebellion.
14 Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu, yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu na Mkombozi wangu.
May you be pleased with the words I speak, and the thoughts I think, Lord my rock and my redeemer.