< Zaburi 19 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, anga zahubiri kazi ya mikono yake.
Unto the end. A Psalm of David. The heavens describe the glory of God, and the firmament announces the work of his hands.
2 Siku baada ya siku zinatoa habari, usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
Day proclaims the word to day, and night to night imparts knowledge.
3 Hakuna msemo wala lugha, ambapo sauti zao hazisikiki.
There are no speeches or conversations, where their voices are not being heard.
4 Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu. Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
Their sound has gone forth through all the earth, and their words to the ends of the world.
5 linafanana na bwana arusi akitoka chumbani mwake, kama shujaa afurahiavyo kukamilisha kushindana kwake.
He has placed his tabernacle in the sun, and he is like a bridegroom coming out of his bedroom. He has exulted like a giant running along the way;
6 Huchomoza upande mmoja wa mbingu, na kufanya mzunguko wake hadi upande mwingine. Hakuna kilichojificha joto lake.
his departure is from the summit of heaven. And his course reaches all the way to its summit. Neither is there anyone who can hide himself from his heat.
7 Sheria ya Bwana ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za Bwana ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.
The law of the Lord is immaculate, converting souls. The testimony of the Lord is faithful, providing wisdom to little ones.
8 Maagizo ya Bwana ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za Bwana huangaza, zatia nuru machoni.
The justice of the Lord is right, rejoicing hearts. The precepts of the Lord are brilliant, enlightening the eyes.
9 Kumcha Bwana ni utakatifu, nako kwadumu milele. Amri za Bwana ni za hakika, nazo zina haki.
The fear of the Lord is holy, enduring for all generations. The judgments of the Lord are true, justified in themselves:
10 Ni za thamani kuliko dhahabu, kuliko dhahabu iliyo safi sana, ni tamu kuliko asali, kuliko asali kutoka kwenye sega.
desirable beyond gold and many precious stones, and sweeter than honey and the honeycomb.
11 Kwa hizo mtumishi wako anaonywa, katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
For, indeed, your servant keeps them, and in keeping them, there are many rewards.
12 Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
Who can understand transgression? From my hidden faults, cleanse me, O Lord,
13 Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi, nazo zisinitawale. Ndipo nitakapokuwa sina lawama, wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.
and from those of others, spare your servant. If they will have no dominion over me, then I will be immaculate, and I will be cleansed from the greatest transgression.
14 Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu, yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu na Mkombozi wangu.
And the eloquence of my mouth will be so as to please, along with the meditation of my heart, in your sight, forever, O Lord, my helper and my redeemer.

< Zaburi 19 >