< Zaburi 19 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, anga zahubiri kazi ya mikono yake.
The heavens declare the glory of God, and the firmament shows his handiwork.
2 Siku baada ya siku zinatoa habari, usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
Day to day utters speech, and night to night shows knowledge.
3 Hakuna msemo wala lugha, ambapo sauti zao hazisikiki.
There is no speech nor language in which their voice is not heard.
4 Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu. Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
Their line has gone out through all the earth, and their words to the end of the world. In them he has set a tabernacle for the sun,
5 linafanana na bwana arusi akitoka chumbani mwake, kama shujaa afurahiavyo kukamilisha kushindana kwake.
which is as a bridegroom coming out of his chamber, and rejoices as a strong man to run his course.
6 Huchomoza upande mmoja wa mbingu, na kufanya mzunguko wake hadi upande mwingine. Hakuna kilichojificha joto lake.
His going forth is from the end of the heavens, and his circuit to the ends of it, and there is nothing hid from the heat of it.
7 Sheria ya Bwana ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za Bwana ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.
The law of Jehovah is perfect, restoring the soul. The testimony of Jehovah is sure, making a simple man wise.
8 Maagizo ya Bwana ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za Bwana huangaza, zatia nuru machoni.
The precepts of Jehovah are right, rejoicing the heart. The commandment of Jehovah is pure, enlightening the eyes.
9 Kumcha Bwana ni utakatifu, nako kwadumu milele. Amri za Bwana ni za hakika, nazo zina haki.
The fear of Jehovah is clean, enduring forever. The ordinances of Jehovah are true, and righteous altogether.
10 Ni za thamani kuliko dhahabu, kuliko dhahabu iliyo safi sana, ni tamu kuliko asali, kuliko asali kutoka kwenye sega.
More to be desired are they than gold, yea, than much fine gold. Sweeter also than honey and the droppings of the honeycomb.
11 Kwa hizo mtumishi wako anaonywa, katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
Moreover by them thy servant is warned. In keeping them there is great reward.
12 Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
Who can discern his errors? Clear thou me from hidden faults.
13 Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi, nazo zisinitawale. Ndipo nitakapokuwa sina lawama, wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.
Keep back thy servant also from presumptuous sins. Let them not have dominion over me. Then I shall be upright, and I shall be clear from great transgression.
14 Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu, yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu na Mkombozi wangu.
Let the words of my mouth and the meditation of my heart be acceptable in thy sight, O Jehovah, my rock, and my redeemer.

< Zaburi 19 >