< Zaburi 18 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana aliyomwimbia Bwana wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli. Alisema hivi: Nakupenda wewe, Ee Bwana, nguvu yangu.
Te amo, oh Señor, mi fortaleza.
2 Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu, Mungu wangu ni mwamba, ambaye kwake ninakimbilia. Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu, ngome yangu.
El Señor es mi roca, y castillo mío y mi libertador; Dios mío, fortaleza mía que me protege, en él pondré mi fe; mi escudo, la fuerza de mi salvación y mi alto refugio.
3 Ninamwita Bwana anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Invocaré mi clamor al Señor, que es digno de ser alabado; así me salvaré de aquellos que están en mi contra.
4 Kamba za mauti zilinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Las cuerdas de la muerte me rodeaban, y los torrentes del mal me aterrorizaron.
5 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol )
Las cuerdas del infierno me rodeaban: las redes de la muerte vinieron sobre mí. (Sheol )
6 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu anisaidie. Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika mbele zake, masikioni mwake.
En mi tribulación invoqué al Señor, mi clamor a mi Dios; Él oyó mi voz en su santo Templo, y mi oración llegó delante de él, hasta sus oídos.
7 Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya milima ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Entonces surgió un gran terremoto en la tierra; y las bases de las montañas se movieron y temblaron, porque estaba enojado.
8 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Le salió humo por la nariz y un fuego de destrucción de su boca; carbones fueron encendidos por él.
9 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
Descorrió la cortina del cielo, para que él pudiera descender; y estaba oscuro bajo sus pies.
10 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
Y se fue volando por el aire, montó en un ser alado: yendo rápidamente en las alas del viento.
11 Alifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika, hema lake kumzunguka, mawingu meusi ya mvua ya angani.
Hizo de la oscuridad su lugar secreto; su tienda de campaña, y a su alrededor eran las aguas oscuras, las espesas nubes de los cielos.
12 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
Por el resplandor de su presencia, brotaron de sus nubes oscuras, granizo y carbones encendidos.
13 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
Jehová hizo tronar en los cielos, y la voz del Altísimo sonó: granizo y carbones de fuego.
14 Aliipiga mishale yake na kutawanya adui, naam, umeme mwingi wa radi na kuwafukuza.
Envió sus flechas, y los dispersó en todas direcciones; lanzó relámpagos y los destruyó.
15 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwako, Ee Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwako.
El fondo del Mar quedó al descubierto, y las bases del mundo fueron descubiertas, a causa de tus palabras de ira, oh Señor, por el aliento de tu boca.
16 Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Tendió su mano desde lo alto, me tomó, y me sacó de las grandes aguas.
17 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
Él me liberó de mi fuerte enemigo, y de aquellos que estaban en mi contra, porque eran más fuertes que yo.
18 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
Vinieron sobre mí en el día de mi angustia; pero el Señor fue mi apoyo.
19 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Él me sacó a un lugar amplio; él fue mi salvador porque se deleitó en mí.
20 Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
El Señor me da la recompensa conforme a mi justicia, porque mis manos están limpias delante de él.
21 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
Porque he guardado los caminos del Señor; No he sido apartado de mi Dios por el pecado.
22 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
Porque todos sus decretos estaban delante de mí, y no aparté sus leyes de mí.
23 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
Y yo me he conducido delante de él sin tacha alguna, y me alejé del pecado.
24 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu machoni pake.
Por esto el Señor me ha dado la recompensa de mi justicia, porque mis manos están limpias en sus presencia.
25 Kwa yeye aliye mwaminifu, unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia, unajionyesha kutokuwa na hatia.
Sobre el que tiene misericordia, tendrás misericordia; con los íntegros serás justo;
26 Kwa aliye mtakatifu, unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka, unajionyesha kuwa mkaidi.
Limpio te mostrarás para con él limpio; pero para el hombre cuyo camino es perverso, serás un juez severo.
27 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini huwashusha wenye kiburi.
Porque tú eres el salvador de los que están en problemas; pero humillas a los orgullosos.
28 Wewe, Ee Bwana, unaifanya taa yangu iendelee kuwaka; Mungu wangu hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Tú, oh Señor, encenderás mi lámpara; por ti, mi Dios, la oscuridad se hará brillante para mí.
29 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
Con tu ayuda atacaré al enemigo; con la ayuda de mi Dios pasaré por los muros de su ciudad.
30 Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu, neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
En cuanto a Dios, su camino es perfecto; la palabra del Señor es probada; él es un escudo para todos los que ponen su fe en él.
31 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Porque ¿quién es Dios sino el Señor? ¿o quién es una Roca sino nuestro Dios?
32 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
Dios me ciñe de poder, guiándome de una manera perfecta.
33 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
El hace mis pies ligeros como de ciervo, y me pone en lugares altos.
34 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
Hace mis manos expertas en guerra, de modo que un arco de bronce se dobla por mis brazos.
35 Hunipa ngao yako ya ushindi, nao mkono wako wa kuume hunitegemeza, unajishusha chini ili kuniinua.
Me diste el escudo de tu salvación; tu diestra ha sido mi sostén, y tu misericordia me ha engrandecido.
36 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Has hecho mis pasos amplios debajo de mí, para que mis pies no se resbalen.
37 Niliwafuatia adui zangu na nikawapata, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Voy detrás de mis enemigos y los alcanzo; no retrocedí hasta que todos estén vencidos.
38 Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
Les daré heridas, para que no puedan levantarse; cayeron debajo de mis pies.
39 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Porque me ceñiste de fuerzas para la batalla; has humillado a los que se oponen a mí.
40 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
Y que delante de mí huyeron. Así pude destruir a los que me aborrecen.
41 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Ellos estaban gritando, pero no había nadie que los ayudara, ni siquiera al Señor, pero él no les dio respuesta.
42 Niliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo; niliwamwaga nje kama tope barabarani.
Entonces fueron aplastados como polvo delante del viento; fueron drenados como el desperdicio de las calles.
43 Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu; umenifanya kuwa kiongozi wa mataifa, watu ambao sikuwajua wananitumikia.
Me has hecho libre de las luchas del pueblo; me has puesto a la cabeza de las naciones; un pueblo del que no tenía conocimiento serán mis siervos.
44 Mara wanisikiapo hunitii, wageni hunyenyekea mbele yangu.
Desde el momento en que mi nombre llegue a sus oídos, ellos me obedecieron: los hombres de otros países se pondrán bajo mi autoridad.
45 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Gente extranjera se acobardó, saldrán de sus lugares secretos temblando de miedo.
46 Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu Mwokozi wangu!
El Señor está vivo; Alabado sea mi Roca, y sea honrado el Dios de mi salvación.
47 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, awatiishaye mataifa chini yangu,
Es Dios quien envía castigo a mis enemigos y pone a los pueblos bajo mi dominio.
48 aniokoaye na adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
Él me hace libre de mis enemigos; de los rebeldes que se alzaron que se enfrentan contra mí; me has liberado del hombre violento.
49 Kwa hiyo nitakusifu katikati ya mataifa, Ee Bwana; nitaliimbia sifa jina lako.
Por esto yo te alabaré, oh Jehová, entre las naciones, y alabaré tu nombre.
50 Humpa mfalme wake ushindi mkuu, huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.
Gran salvación le da a su rey; Él tiene misericordia del rey su ungido, David, y de su simiente para siempre.