< Zaburi 18 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana aliyomwimbia Bwana wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli. Alisema hivi: Nakupenda wewe, Ee Bwana, nguvu yangu.
Amarte he, Jehová, fortaleza mía.
2 Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu, Mungu wangu ni mwamba, ambaye kwake ninakimbilia. Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu, ngome yangu.
Jehová, roca mía, y castillo mío, y escapador mío; Dios mío, fuerte mío: confiarme he en él: escudo mío, y el cuerno de mi salud; refugio mío.
3 Ninamwita Bwana anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Al alabado Jehová invocaré, y seré salvo de mis enemigos.
4 Kamba za mauti zilinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Cercáronme dolores de muerte, y arroyos de perversidad me atemorizaron:
5 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol )
Dolores del sepulcro me rodearon; anticipáronme lazos de muerte: (Sheol )
6 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu anisaidie. Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika mbele zake, masikioni mwake.
En mi angustia llamé a Jehová, y clamé a mi Dios: él oyó desde su templo mi voz, y mi clamor entró delante de él, en sus orejas.
7 Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya milima ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Y la tierra fue conmovida y tembló: y los fundamentos de los montes se estremecieron, y se removieron, porque él se enojó.
8 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Subió humo en su nariz, y de su boca fuego quemante: carbones se encendieron de él.
9 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
Y abajó los cielos, y descendió; y oscuridad debajo de sus pies.
10 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
Y cabalgó sobre un querubín, y voló: y voló sobre las alas del viento.
11 Alifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika, hema lake kumzunguka, mawingu meusi ya mvua ya angani.
Puso tinieblas por su escondedero: en sus en derredores de su tabernáculo, oscuridad de aguas, nubes de los cielos.
12 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
Por el resplandor de delante de él sus nubes pasaron: granizo y carbones de fuego.
13 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
Y tronó en los cielos Jehová, y el Altísimo dio su voz: granizo y carbones de fuego.
14 Aliipiga mishale yake na kutawanya adui, naam, umeme mwingi wa radi na kuwafukuza.
Y envió sus saetas y desbaratólos: y echó relámpagos, y los destruyó.
15 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwako, Ee Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwako.
Y aparecieron las honduras de las aguas: y descubriéronse los cimientos del mundo por tu reprensión, o! Jehová, por el soplo del viento de tu nariz.
16 Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Envió desde lo alto, me tomó, me sacó de las muchas aguas.
17 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
Me escapó de mi fuerte enemigo, y de los que me aborrecieron: aunque ellos eran más fuertes que yo.
18 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
Anticipáronme en el día de mi quebrantamiento: mas Jehová me fue por bordón.
19 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Y me sacó a anchura: me libró, porque se agradó de mí.
20 Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
Jehová me pagará conforme a mi justicia: conforme a la limpieza de mis manos me volverá.
21 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
Por cuanto guardé los caminos de Jehová: y no me maleé con mi Dios.
22 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
Porque todos sus juicios estuvieron delante de mí: y no eché de mí sus estatutos.
23 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
Y fui perfecto con él: y me recaté de mi maldad.
24 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu machoni pake.
Y pagóme Jehová conforme a mi justicia: conforme a la limpieza de mis manos delante de sus ojos.
25 Kwa yeye aliye mwaminifu, unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia, unajionyesha kutokuwa na hatia.
Con el misericordioso serás misericordioso: y con el varón perfecto serás perfecto.
26 Kwa aliye mtakatifu, unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka, unajionyesha kuwa mkaidi.
Con el limpio serás limpio, y con el perverso serás perverso.
27 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini huwashusha wenye kiburi.
Por tanto tú al pueblo humilde salvarás: y los ojos altivos humillarás.
28 Wewe, Ee Bwana, unaifanya taa yangu iendelee kuwaka; Mungu wangu hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Por tanto tú alumbrarás mi candela: Jehová, mi Dios, alumbrará mis tinieblas,
29 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
Porque contigo desharé ejércitos: y en mi Dios asaltaré muros.
30 Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu, neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
Dios, perfecto su camino: la palabra de Jehová afinada: escudo es a todos los que esperan en él.
31 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Porque ¿qué Dios hay fuera de Jehová? ¿y qué fuerte fuera de nuestro Dios?
32 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
Dios, que me ciñe de fuerza; e hizo perfecto mi camino:
33 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
Que pone mis pies como pies de ciervas: y me hizo estar sobre mis alturas:
34 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
Que enseña mis manos para la batalla; y el arco de acero será quebrado con mis brazos.
35 Hunipa ngao yako ya ushindi, nao mkono wako wa kuume hunitegemeza, unajishusha chini ili kuniinua.
Y me diste el escudo de tu salud; y tu diestra me sustentará, y tu mansedumbre me multiplicará.
36 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Ensancharás mi paso debajo de mí, y no titubearán mis rodillas.
37 Niliwafuatia adui zangu na nikawapata, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Perseguiré mis enemigos, y alcanzarles he; y no volveré hasta acabarles.
38 Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
Herírles he, y no podrán levantarse: caerán debajo de mis pies.
39 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Y ceñísteme de fortaleza para la pelea: agobiaste mis enemigos debajo de mí.
40 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
Y dísteme la cerviz de mis enemigos: y a los que me aborrecían, destruí.
41 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Clamaron, y no hubo quien salvase: a Jehová, mas no les oyó.
42 Niliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo; niliwamwaga nje kama tope barabarani.
Y los molí como polvo delante del viento: como a lodo de las calles los esparcí.
43 Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu; umenifanya kuwa kiongozi wa mataifa, watu ambao sikuwajua wananitumikia.
Librásteme de contiendas de pueblo: pusísteme por cabecera de gentes; pueblo que no conocí, me sirvió.
44 Mara wanisikiapo hunitii, wageni hunyenyekea mbele yangu.
A oída de oreja me obedeció: los hombres extraños me mintieron.
45 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Los hombres extraños se cayeron: y tuvieron miedo desde sus encerramientos.
46 Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu Mwokozi wangu!
Viva Jehová, y bendito sea mi fuerte: y sea ensalzado el Dios de mi salud.
47 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, awatiishaye mataifa chini yangu,
El Dios que me da las venganzas, y sujetó pueblos debajo de mí.
48 aniokoaye na adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
Mi librador de mis enemigos: también me hiciste superior de mis adversarios: de varón violento me libraste.
49 Kwa hiyo nitakusifu katikati ya mataifa, Ee Bwana; nitaliimbia sifa jina lako.
Por tanto yo te confesaré entre las gentes, o! Jehová, y cantaré a tu nombre.
50 Humpa mfalme wake ushindi mkuu, huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.
Que engrandece las saludes de su rey, y que hace misericordia a su ungido David, y a su simiente para siempre.