< Zaburi 18 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana aliyomwimbia Bwana wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli. Alisema hivi: Nakupenda wewe, Ee Bwana, nguvu yangu.
Načelniku godbe, Davida hlapca Gospodovega; kateri je govoril Gospodu té pesmi besede v dan, ko ga je bil rešil Gospod iz roke vseh sovražnikov njegovih, kakor iz roke Savlove. In rekel je: Iz osrčja svojega bodem te ljubil, Gospod, moja krepost.
2 Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu, Mungu wangu ni mwamba, ambaye kwake ninakimbilia. Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu, ngome yangu.
Gospod, skala moja in grad moj in rešitelj moj; Bog mogočni moj, pečina moja, kamor pribegam, ščit moj in blaginje moje rog, višina moja.
3 Ninamwita Bwana anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Hvaljenega kličem Gospoda in rešujem se sovražnikov svojih.
4 Kamba za mauti zilinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Obdajajo me smrtne bolečine in malopridnih hudourniki me strašijo.
5 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
Groba bolečine me obhajajo, smrtne zanke so mi na poti. (Sheol h7585)
6 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu anisaidie. Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika mbele zake, masikioni mwake.
V stiski svoji kličem Gospoda, in do Boga svojega vpijem; iz svetišča svojega usliši moj glas, in vpitje moje predenj pride do ušes njegovih:
7 Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya milima ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
In stresa se in giblje zemlja, in podloge gorâ se majó; stresajo se pa, ko se mu vname jeza.
8 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Dim se vali skozi nos njegov in ogenj požrešen iz ust njegovih; žarjavica goreča gre od njega.
9 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
In nagne nebo ter stopi dol, z mrakom pod svojimi nogami,
10 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
In sedeč na kerubih leti, in plava na vétrovih perotih.
11 Alifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika, hema lake kumzunguka, mawingu meusi ya mvua ya angani.
Temo si napravi v zavetje svoje, okolo sebe za šator svoj; temotne vode, gošče gornjih oblakov.
12 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
Od svita pred njim prehajajo gosti oblaki njegovi, toča in žarjavica ognjena.
13 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
Na nebesih grmi Gospod in z višave izhaja glas njegov, toča in žarjavica ognjena.
14 Aliipiga mishale yake na kutawanya adui, naam, umeme mwingi wa radi na kuwafukuza.
Tako proži pušice svoje, razsipa jih in strele meče ter jih podi.
15 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwako, Ee Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwako.
Prikazujejo se tudi najnižje struge vodâ, in razgrinjajo se podloge vesoljne zemlje od hudovanja tvojega, Gospod, od sape tvojega nosú.
16 Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Iz višine poseže ter me potegne gor, izvleče me iz mnogih vodâ.
17 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
Reši me neprijatelja mojega močnejšega, in sovražnikov mojih, ko so krepkejši od mene.
18 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
Srečujejo me ob času nadloge moje, tedaj mi je za palico Gospod:
19 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
In izpelje me na prosto; reši me, ker me ima rad.
20 Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
Podeljuje mi Gospod po pravičnosti moji; po čistosti mojih rok mi povrača.
21 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
Ker se držim potov Gospodovih, ter se ne obračam krivično od svojega Boga;
22 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
Ker so vse sodbe njegove pred mojimi očmi; in postav njegovih ne odvračam od sebe:
23 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
Ker sem pošten pred njim, in se varujem, da ne ravnam krivično.
24 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu machoni pake.
Povrača mi Gospod po pravičnosti moji; po čistosti mojih rok pred njegovimi očmi.
25 Kwa yeye aliye mwaminifu, unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia, unajionyesha kutokuwa na hatia.
Z dobrotljivim izkazuješ se dobrotljivega, s poštenim možem izkazuješ se poštenega.
26 Kwa aliye mtakatifu, unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka, unajionyesha kuwa mkaidi.
S čistim kažeš se čistega, ali popačenemu nasprotuješ.
27 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini huwashusha wenye kiburi.
Ker ti otimaš ljudstvo ubogo, prevzetne pa oči ponižuješ.
28 Wewe, Ee Bwana, unaifanya taa yangu iendelee kuwaka; Mungu wangu hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Dà, svetilo moje razsvetljuješ; Gospod, moj Bog razjasnjuje moje temé.
29 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
S teboj namreč prodiram skozi krdelo, in z Bogom svojim preskakujem zid.
30 Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu, neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
Tega Boga mogočnega pot je poštena; govor Gospodov ves čist; ščit je vsem, kateri pribegajo k njemu.
31 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Ker kdo je Bog razen Gospod? in kdo skala razen naš Bog?
32 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
Ta je Bog mogočni, ki me opasuje z močjo, in dela pošteno mojo pot:
33 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
Storivši noge moje kakor jelenom, da me stavi na višino mojo;
34 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
Boja uči roke moje; tako da zlomi lok jekleni roka moja.
35 Hunipa ngao yako ya ushindi, nao mkono wako wa kuume hunitegemeza, unajishusha chini ili kuniinua.
Ker daješ mi ščit blaginje svoje, in desnica tvoja me podpira, in krotkost tvoja me povišuje.
36 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Hoji moji razširjaš prostor moj; in členki mojih nog ne omahujejo.
37 Niliwafuatia adui zangu na nikawapata, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Sovražnike svoje podim in dohajam jih; in ne povrnem se, dokler jih nisem uničil.
38 Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
Zdrobim jih tako, da ne morejo več vstati, padajoč pod noge moje.
39 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Opasuješ me namreč z močjo za vojsko; pod me podiraš nje, ki se spenjajo zoper mene.
40 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
In neprijateljev mojih tilnik mi podajaš; da ugonobim sovražnike svoje.
41 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Vpijejo, a ni ga, da jih reši; h Gospodu, a ne usliši jih.
42 Niliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo; niliwamwaga nje kama tope barabarani.
Zatorej jih razmeljem kakor prah pred vetrom; kakor blato na ulicah jih drobim.
43 Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu; umenifanya kuwa kiongozi wa mataifa, watu ambao sikuwajua wananitumikia.
Oproščaš me prepirov ljudstva; staviš me narodom na čelo; ljudstvo, katerega nisem poznal, služi mi:
44 Mara wanisikiapo hunitii, wageni hunyenyekea mbele yangu.
Na sluh ušesa so mi pokorni; tujci se mi udajajo lažnjivo;
45 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Tujci padajo in pritrepetavajo iz gradov svojih.
46 Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu Mwokozi wangu!
Gospod živi in blagoslovljena skala moja; zatorej naj se povišuje Bog blaginje moje.
47 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, awatiishaye mataifa chini yangu,
Bog ta mogočni, ki mi daje maščevanje, in spravlja ljudstva pód me;
48 aniokoaye na adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
Rešuje me sovražnikov mojih; tudi nad nje, ki se spenjajo zoper mene, povzdignil si me; možu silovitemu si me iztrgal.
49 Kwa hiyo nitakusifu katikati ya mataifa, Ee Bwana; nitaliimbia sifa jina lako.
Zatorej te bodem slavil med narodi, Gospod, in prepeval bodem tvojemu imenu:
50 Humpa mfalme wake ushindi mkuu, huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.
Da veliko blaginjo vsakoršno podeljuješ svojemu kralju, in izkazuješ milost maziljencu svojemu, Davidu in semenu njegovemu na veke.

< Zaburi 18 >