< Zaburi 18 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana aliyomwimbia Bwana wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli. Alisema hivi: Nakupenda wewe, Ee Bwana, nguvu yangu.
Eu te amarei do coração, ó Senhor, fortaleza minha.
2 Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu, Mungu wangu ni mwamba, ambaye kwake ninakimbilia. Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu, ngome yangu.
O Senhor é o meu rochedo, e o meu logar forte e o meu libertador; o meu Deus, a minha fortaleza, em quem confio, o meu escudo, a força da minha salvação, e o meu alto refugio.
3 Ninamwita Bwana anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Invocarei o nome do Senhor, que é digno de louvor, e ficarei livre dos meus inimigos.
4 Kamba za mauti zilinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Tristezas de morte me cercaram, e torrentes de impiedade me assombraram.
5 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
Tristezas do inferno me cingiram, laços de morte me surprehenderam. (Sheol h7585)
6 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu anisaidie. Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika mbele zake, masikioni mwake.
Na angustia invoquei ao Senhor, e clamei ao meu Deus: desde o seu templo ouviu a minha voz, aos seus ouvidos chegou o meu clamor perante a sua face.
7 Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya milima ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Então a terra se abalou e tremeu; e os fundamentos dos montes tambem se moveram e se abalaram, porquanto se indignou.
8 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Do seu nariz subiu fumo, e da sua bocca saiu fogo que consumia; carvões se accenderam d'elle.
9 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
Abaixou os céus, e desceu, e a escuridão estava debaixo de seus pés.
10 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
E montou n'um cherubim, e voou; sim, voou sobre as azas do vento.
11 Alifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika, hema lake kumzunguka, mawingu meusi ya mvua ya angani.
Fez das trevas o seu logar occulto; o pavilhão que o cercava era a escuridão das aguas e as nuvens dos céus.
12 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
Ao resplandor da sua presença as nuvens se espalharam; a saraiva e as brazas de fogo.
13 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
E o Senhor trovejou nos céus, o Altissimo levantou a sua voz; a saraiva e as brazas de fogo.
14 Aliipiga mishale yake na kutawanya adui, naam, umeme mwingi wa radi na kuwafukuza.
Despediu as suas settas, e os espalhou: multiplicou raios, e os perturbou.
15 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwako, Ee Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwako.
Então foram vistas as profundezas das aguas, e foram descobertos os fundamentos do mundo; pela tua reprehensão. Senhor, ao sopro do vento dos teus narizes.
16 Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Enviou desde o alto, e me tomou: tirou-me das muitas aguas.
17 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
Livrou-me do meu inimigo forte e dos que me aborreciam, pois eram mais poderosos do que eu.
18 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
Surprehenderam-me no dia da minha calamidade; mas o Senhor foi o meu encosto.
19 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Trouxe-me para um logar espaçoso; livrou-me, porque tinha prazer em mim.
20 Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
Recompensou-me o Senhor conforme a minha justiça, retribuiu-me conforme a pureza das minhas mãos.
21 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
Porque guardei os caminhos do Senhor, e não me apartei impiamente do meu Deus.
22 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
Porque todos os seus juizos estavam diante de mim, e não rejeitei os seus estatutos.
23 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
Tambem fui sincero perante elle, e me guardei da minha iniquidade.
24 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu machoni pake.
Portanto retribuiu-me o Senhor conforme a minha justiça, conforme a pureza de minhas mãos perante os seus olhos.
25 Kwa yeye aliye mwaminifu, unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia, unajionyesha kutokuwa na hatia.
Com o benigno te mostrarás benigno; e com o homem sincero te mostrarás sincero;
26 Kwa aliye mtakatifu, unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka, unajionyesha kuwa mkaidi.
Com o puro te mostrarás puro; e com o perverso te mostrarás indomavel.
27 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini huwashusha wenye kiburi.
Porque tu livrarás ao povo afflicto, e abaterás os olhos altivos.
28 Wewe, Ee Bwana, unaifanya taa yangu iendelee kuwaka; Mungu wangu hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Porque tu accenderás a minha candeia; o Senhor meu Deus allumiará as minhas trevas.
29 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
Porque comtigo entrei pelo meio d'um esquadrão, com o meu Deus saltei uma muralha.
30 Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu, neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
O caminho de Deus é perfeito; a palavra do Senhor é provada: é um escudo para todos os que n'elle confiam.
31 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Porque quem é Deus senão o Senhor? e quem é rochedo senão o nosso Deus?
32 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
Deus é o que me cinge de força e aperfeiçoa o meu caminho.
33 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
Faz os meus pés como os das cervas, e põe-me nas minhas alturas.
34 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
Ensina as minhas mãos para a guerra, de sorte que os meus braços quebraram um arco de cobre.
35 Hunipa ngao yako ya ushindi, nao mkono wako wa kuume hunitegemeza, unajishusha chini ili kuniinua.
Tambem me déste o escudo da tua salvação: a tua mão direita me susteve, e a tua mansidão me engrandeceu.
36 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Alargaste os meus passos debaixo de mim, de maneira que os meus artelhos não vacillaram.
37 Niliwafuatia adui zangu na nikawapata, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Persegui os meus inimigos, e os alcancei: não voltei senão depois de os ter consumido.
38 Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
Atravessei-os, de sorte que não se poderam levantar: cairam debaixo dos meus pés.
39 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Pois me cingiste de força para a peleja: fizeste abater debaixo de mim aquelles que contra mim se levantaram.
40 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
Déste-me tambem o pescoço dos meus inimigos para que eu podesse destruir os que me aborrecem.
41 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Clamaram, mas não houve quem os livrasse: até ao Senhor, mas elle não lhes respondeu.
42 Niliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo; niliwamwaga nje kama tope barabarani.
Então os esmiucei como o pó diante do vento; deitei-os fóra como a lama das ruas.
43 Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu; umenifanya kuwa kiongozi wa mataifa, watu ambao sikuwajua wananitumikia.
Livraste-me das contendas do povo, e me fizeste cabeça das nações; um povo que não conheci, me servirá.
44 Mara wanisikiapo hunitii, wageni hunyenyekea mbele yangu.
Em ouvindo a minha voz, me obedecerão: os estranhos se submetterão a mim.
45 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Os estranhos decairão, e terão medo nos seus encerramentos.
46 Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu Mwokozi wangu!
O Senhor vive: e bemdito seja o meu rochedo, e exaltado seja o Deus da minha salvação.
47 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, awatiishaye mataifa chini yangu,
É Deus que me vinga inteiramente, e sujeita os povos debaixo de mim;
48 aniokoaye na adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
O que me livra de meus inimigos; --sim, tu me exaltas sobre os que se levantam contra mim, tu me livras do homem violento.
49 Kwa hiyo nitakusifu katikati ya mataifa, Ee Bwana; nitaliimbia sifa jina lako.
Pelo que, ó Senhor, te louvarei entre as nações, e cantarei louvores ao teu nome.
50 Humpa mfalme wake ushindi mkuu, huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.
Pois engrandece a salvação do teu rei, e usa de benignidade com o seu ungido, com David, e com a sua semente para sempre.

< Zaburi 18 >