< Zaburi 18 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana aliyomwimbia Bwana wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli. Alisema hivi: Nakupenda wewe, Ee Bwana, nguvu yangu.
Til sangmesteren; av Herrens tjener David, som talte denne sangs ord til Herren den dag da Herren hadde utfridd ham av alle hans fienders hånd og av Sauls hånd. Og han sa: Herre, jeg har dig hjertelig kjær, min styrke!
2 Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu, Mungu wangu ni mwamba, ambaye kwake ninakimbilia. Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu, ngome yangu.
Herren er min klippe og min festning og min frelser; min Gud er min klippe, som jeg setter min lit til, mitt skjold og min frelses horn, min borg.
3 Ninamwita Bwana anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Jeg påkaller den Høilovede, Herren, og blir frelst fra mine fiender.
4 Kamba za mauti zilinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Dødens rep omspente mig, og fordervelsens strømmer forferdet mig.
5 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol )
Dødsrikets rep omgav mig, dødens snarer overfalt mig. (Sheol )
6 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu anisaidie. Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika mbele zake, masikioni mwake.
I min trengsel påkalte jeg Herren, og jeg ropte til min Gud; han hørte fra sitt tempel min røst, og mitt skrik kom for ham, til hans ører.
7 Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya milima ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Da rystet og bevet jorden, og fjellenes grunnvoller skalv, og de rystet, for hans vrede var optendt.
8 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Det steg røk op av hans nese, og fortærende ild fra hans munn; glør brente ut av ham.
9 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
Og han bøide himmelen og steg ned, og det var mørke under hans føtter.
10 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
Og han fór på kjeruber og fløi, og han fór hastig frem på vindens vinger.
11 Alifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika, hema lake kumzunguka, mawingu meusi ya mvua ya angani.
Han gjorde mørke til sitt dekke, rundt omkring sig til sitt skjul, mørke vann, tykke skyer.
12 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
Frem av glansen foran ham fór hans skyer frem, hagl og gloende kull.
13 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
Og Herren tordnet i himmelen, den Høieste lot sin røst høre, hagl og gloende kull.
14 Aliipiga mishale yake na kutawanya adui, naam, umeme mwingi wa radi na kuwafukuza.
Og han utsendte sine piler og spredte dem omkring - lyn i mengde og forvirret dem.
15 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwako, Ee Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwako.
Da kom vannenes strømmer til syne, og jordens grunnvoller blev avdekket ved din trusel, Herre, for din neses åndepust.
16 Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Han rakte sin hånd ut fra det høie, han grep mig; han drog mig op av store vann.
17 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
Han fridde mig ut fra min sterke fiende og fra mine avindsmenn; for de var mig for mektige.
18 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
De overfalt mig på min motgangs dag; men Herren blev min støtte.
19 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Og han førte mig ut i fritt rum; han frelste mig, for han hadde behag i mig.
20 Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
Herren gjengjeldte mig efter min rettferdighet, han betalte mig efter mine henders renhet.
21 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
For jeg tok vare på Herrens veier og vek ikke i ondskap fra min Gud.
22 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
For alle hans lover hadde jeg for øie, og hans bud lot jeg ikke vike fra mig.
23 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
Og jeg var ulastelig for ham og voktet mig vel for min synd.
24 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu machoni pake.
Og Herren gjengjeldte mig efter min rettferdighet, efter mine henders renhet for hans øine.
25 Kwa yeye aliye mwaminifu, unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia, unajionyesha kutokuwa na hatia.
Mot den fromme viser du dig from, mot den rettvise mann viser du dig rettvis,
26 Kwa aliye mtakatifu, unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka, unajionyesha kuwa mkaidi.
mot den rene viser du dig ren, mot den forvendte viser du dig vrang.
27 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini huwashusha wenye kiburi.
For du frelser elendige folk, og du fornedrer høie øine.
28 Wewe, Ee Bwana, unaifanya taa yangu iendelee kuwaka; Mungu wangu hulifanya giza langu kuwa mwanga.
For du lar min lampe skinne; Herren min Gud opklarer mitt mørke.
29 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
For ved dig stormer jeg løs på fiendeskarer, og ved min Gud springer jeg over murer.
30 Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu, neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
Gud, hans vei er fullkommen; Herrens ord er rent, han er et skjold for alle dem som setter sin lit til ham.
31 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
For hvem er Gud foruten Herren, og hvem er en klippe, uten vår Gud?
32 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
Den Gud som omgjorder mig med kraft og gjør min vei fri for støt,
33 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
som gir mig føtter likesom hindene og stiller mig på mine høider,
34 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
som oplærer mine hender til krig, så mine armer spenner kobberbuen.
35 Hunipa ngao yako ya ushindi, nao mkono wako wa kuume hunitegemeza, unajishusha chini ili kuniinua.
Og du gir mig din frelse til skjold, og din høire hånd støtter mig, og din mildhet gjør mig stor.
36 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Du gjør rummet vidt for mine skritt under mig, og mine ankler vakler ikke.
37 Niliwafuatia adui zangu na nikawapata, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Jeg forfølger mine fiender og når dem, og jeg vender ikke tilbake før jeg har gjort ende på dem.
38 Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
Jeg knuser dem, så de ikke makter å reise sig; de faller under mine føtter.
39 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Og du omgjorder mig med kraft til krig, du bøier mine motstandere under mig.
40 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
Og mine fiender lar du vende mig ryggen, og mine avindsmenn utrydder jeg.
41 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
De roper, men der er ingen frelser - til Herren, men han svarer dem ikke.
42 Niliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo; niliwamwaga nje kama tope barabarani.
Og jeg knuser dem som støv for vinden, jeg tømmer dem ut som søle på gatene.
43 Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu; umenifanya kuwa kiongozi wa mataifa, watu ambao sikuwajua wananitumikia.
Du redder mig fra folkekamper, du setter mig til hode for hedninger; folkeferd som jeg ikke kjenmer, tjener mig.
44 Mara wanisikiapo hunitii, wageni hunyenyekea mbele yangu.
Bare de hører om mig, blir de mig lydige; fremmede kryper for mig.
45 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Fremmede visner bort og går bevende ut av sine borger.
46 Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu Mwokozi wangu!
Herren lever, og priset er min klippe, og ophøiet er min frelses Gud,
47 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, awatiishaye mataifa chini yangu,
den Gud som gir mig hevn og legger folkeferd under mig,
48 aniokoaye na adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
som frir mig ut fra mine fiender; ja, over mine motstandere ophøier du mig, fra voldsmannen redder du mig.
49 Kwa hiyo nitakusifu katikati ya mataifa, Ee Bwana; nitaliimbia sifa jina lako.
Derfor vil jeg prise dig iblandt hedningene, Herre, og lovsynge ditt navn.
50 Humpa mfalme wake ushindi mkuu, huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.
Han gjør frelsen stor for sin konge, han gjør miskunnhet mot sin salvede, mot David og mot hans ætt til evig tid.