< Zaburi 18 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana aliyomwimbia Bwana wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli. Alisema hivi: Nakupenda wewe, Ee Bwana, nguvu yangu.
Al maestro del coro. Di Davide, servo del Signore, che rivolse al Signore le parole di questo canto, quando il Signore lo liberò dal potere di tutti i suoi nemici, Ti amo, Signore, mia forza,
2 Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu, Mungu wangu ni mwamba, ambaye kwake ninakimbilia. Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu, ngome yangu.
Signore, mia roccia, mia fortezza, mio liberatore; mio Dio, mia rupe, in cui trovo riparo; mio scudo e baluardo, mia potente salvezza.
3 Ninamwita Bwana anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Invoco il Signore, degno di lode, e sarò salvato dai miei nemici.
4 Kamba za mauti zilinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Mi circondavano flutti di morte, mi travolgevano torrenti impetuosi;
5 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
gia mi avvolgevano i lacci degli inferi, gia mi stringevano agguati mortali. (Sheol h7585)
6 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu anisaidie. Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika mbele zake, masikioni mwake.
Nel mio affanno invocai il Signore, nell'angoscia gridai al mio Dio: dal suo tempio ascoltò la mia voce, al suo orecchio pervenne il mio grido.
7 Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya milima ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
La terra tremò e si scosse; vacillarono le fondamenta dei monti, si scossero perché egli era sdegnato.
8 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Dalle sue narici saliva fumo, dalla sua bocca un fuoco divorante; da lui sprizzavano carboni ardenti.
9 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
Abbassò i cieli e discese, fosca caligine sotto i suoi piedi.
10 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
Cavalcava un cherubino e volava, si librava sulle ali del vento.
11 Alifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika, hema lake kumzunguka, mawingu meusi ya mvua ya angani.
Si avvolgeva di tenebre come di velo, acque oscure e dense nubi lo coprivano.
12 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
Davanti al suo fulgore si dissipavano le nubi con grandine e carboni ardenti.
13 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
Il Signore tuonò dal cielo, l'Altissimo fece udire la sua voce: grandine e carboni ardenti.
14 Aliipiga mishale yake na kutawanya adui, naam, umeme mwingi wa radi na kuwafukuza.
Scagliò saette e li disperse, fulminò con folgori e li sconfisse.
15 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwako, Ee Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwako.
Allora apparve il fondo del mare, si scoprirono le fondamenta del mondo, per la tua minaccia, Signore, per lo spirare del tuo furore.
16 Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Stese la mano dall'alto e mi prese, mi sollevò dalle grandi acque,
17 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
mi liberò da nemici potenti, da coloro che mi odiavano ed eran più forti di me.
18 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
Mi assalirono nel giorno di sventura, ma il Signore fu mio sostegno;
19 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
mi portò al largo, mi liberò perché mi vuol bene.
20 Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
Il Signore mi tratta secondo la mia giustizia, mi ripaga secondo l'innocenza delle mie mani;
21 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
perché ho custodito le vie del Signore, non ho abbandonato empiamente il mio Dio.
22 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
I suoi giudizi mi stanno tutti davanti, non ho respinto da me la sua legge;
23 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
ma integro sono stato con lui e mi sono guardato dalla colpa.
24 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu machoni pake.
Il Signore mi rende secondo la mia giustizia, secondo l'innocenza delle mie mani davanti ai suoi occhi.
25 Kwa yeye aliye mwaminifu, unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia, unajionyesha kutokuwa na hatia.
Con l'uomo buono tu sei buono con l'uomo integro tu sei integro,
26 Kwa aliye mtakatifu, unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka, unajionyesha kuwa mkaidi.
con l'uomo puro tu sei puro, con il perverso tu sei astuto.
27 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini huwashusha wenye kiburi.
Perché tu salvi il popolo degli umili, ma abbassi gli occhi dei superbi.
28 Wewe, Ee Bwana, unaifanya taa yangu iendelee kuwaka; Mungu wangu hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Tu, Signore, sei luce alla mia lampada; il mio Dio rischiara le mie tenebre.
29 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
Con te mi lancerò contro le schiere, con il mio Dio scavalcherò le mura.
30 Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu, neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
La via di Dio è diritta, la parola del Signore è provata al fuoco; egli è scudo per chi in lui si rifugia.
31 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Infatti, chi è Dio, se non il Signore? O chi è rupe, se non il nostro Dio?
32 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
Il Dio che mi ha cinto di vigore e ha reso integro il mio cammino;
33 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
mi ha dato agilità come di cerve, sulle alture mi ha fatto stare saldo;
34 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
ha addestrato le mie mani alla battaglia, le mie braccia a tender l'arco di bronzo.
35 Hunipa ngao yako ya ushindi, nao mkono wako wa kuume hunitegemeza, unajishusha chini ili kuniinua.
Tu mi hai dato il tuo scudo di salvezza, la tua destra mi ha sostenuto, la tua bontà mi ha fatto crescere.
36 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Hai spianato la via ai miei passi, i miei piedi non hanno vacillato.
37 Niliwafuatia adui zangu na nikawapata, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Ho inseguito i miei nemici e li ho raggiunti, non sono tornato senza averli annientati.
38 Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
Li ho colpiti e non si sono rialzati, sono caduti sotto i miei piedi.
39 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Tu mi hai cinto di forza per la guerra, hai piegato sotto di me gli avversari.
40 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
Dei nemici mi hai mostrato le spalle, hai disperso quanti mi odiavano.
41 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Hanno gridato e nessuno li ha salvati, al Signore, ma non ha risposto.
42 Niliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo; niliwamwaga nje kama tope barabarani.
Come polvere al vento li ho dispersi, calpestati come fango delle strade.
43 Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu; umenifanya kuwa kiongozi wa mataifa, watu ambao sikuwajua wananitumikia.
Mi hai scampato dal popolo in rivolta, mi hai posto a capo delle nazioni. Un popolo che non conoscevo mi ha servito;
44 Mara wanisikiapo hunitii, wageni hunyenyekea mbele yangu.
all'udirmi, subito mi obbedivano, stranieri cercavano il mio favore,
45 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
impallidivano uomini stranieri e uscivano tremanti dai loro nascondigli.
46 Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu Mwokozi wangu!
Viva il Signore e benedetta la mia rupe, sia esaltato il Dio della mia salvezza.
47 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, awatiishaye mataifa chini yangu,
Dio, tu mi accordi la rivincita e sottometti i popoli al mio giogo,
48 aniokoaye na adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
mi scampi dai nemici furenti, dei miei avversari mi fai trionfare e mi liberi dall'uomo violento.
49 Kwa hiyo nitakusifu katikati ya mataifa, Ee Bwana; nitaliimbia sifa jina lako.
Per questo, Signore, ti loderò tra i popoli e canterò inni di gioia al tuo nome.
50 Humpa mfalme wake ushindi mkuu, huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.
Egli concede al suo re grandi vittorie, si mostra fedele al suo consacrato, a Davide e alla sua discendenza per sempre.

< Zaburi 18 >