< Zaburi 18 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana aliyomwimbia Bwana wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli. Alisema hivi: Nakupenda wewe, Ee Bwana, nguvu yangu.
למנצח לעבד יהוה--לדוד אשר דבר ליהוה את-דברי השירה הזאת-- ביום הציל-יהוה אותו מכף כל-איביו ומיד שאול ב ויאמר-- ארחמך יהוה חזקי
2 Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu, Mungu wangu ni mwamba, ambaye kwake ninakimbilia. Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu, ngome yangu.
יהוה סלעי ומצודתי-- ומפלטי אלי צורי אחסה-בו מגני וקרן-ישעי משגבי
3 Ninamwita Bwana anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
מהלל אקרא יהוה ומן-איבי אושע
4 Kamba za mauti zilinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
אפפוני חבלי-מות ונחלי בליעל יבעתוני
5 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
חבלי שאול סבבוני קדמוני מוקשי מות (Sheol h7585)
6 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu anisaidie. Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika mbele zake, masikioni mwake.
בצר-לי אקרא יהוה-- ואל-אלהי אשוע ישמע מהיכלו קולי ושועתי לפניו תבוא באזניו
7 Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya milima ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
ותגעש ותרעש הארץ-- ומוסדי הרים ירגזו ויתגעשו כי-חרה לו
8 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
עלה עשן באפו-- ואש-מפיו תאכל גחלים בערו ממנו
9 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
ויט שמים וירד וערפל תחת רגליו
10 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
וירכב על-כרוב ויעף וידא על-כנפי-רוח
11 Alifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika, hema lake kumzunguka, mawingu meusi ya mvua ya angani.
ישת חשך סתרו-- סביבותיו סכתו חשכת-מים עבי שחקים
12 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
מנגה נגדו עביו עברו--ברד וגחלי-אש
13 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
וירעם בשמים יהוה--ועליון יתן קלו ברד וגחלי-אש
14 Aliipiga mishale yake na kutawanya adui, naam, umeme mwingi wa radi na kuwafukuza.
וישלח חציו ויפיצם וברקים רב ויהמם
15 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwako, Ee Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwako.
ויראו אפיקי מים ויגלו מוסדות תבל מגערתך יהוה-- מנשמת רוח אפך
16 Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
ישלח ממרום יקחני ימשני ממים רבים
17 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
יצילני מאיבי עז ומשנאי כי-אמצו ממני
18 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
יקדמוני ביום-אידי ויהי-יהוה למשען לי
19 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
ויוציאני למרחב יחלצני כי חפץ בי
20 Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
יגמלני יהוה כצדקי כבר ידי ישיב לי
21 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
כי-שמרתי דרכי יהוה ולא-רשעתי מאלהי
22 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
כי כל-משפטיו לנגדי וחקתיו לא-אסיר מני
23 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
ואהי תמים עמו ואשתמר מעוני
24 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu machoni pake.
וישב-יהוה לי כצדקי כבר ידי לנגד עיניו
25 Kwa yeye aliye mwaminifu, unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia, unajionyesha kutokuwa na hatia.
עם-חסיד תתחסד עם-גבר תמים תתמם
26 Kwa aliye mtakatifu, unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka, unajionyesha kuwa mkaidi.
עם-נבר תתברר ועם-עקש תתפתל
27 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini huwashusha wenye kiburi.
כי-אתה עם-עני תושיע ועינים רמות תשפיל
28 Wewe, Ee Bwana, unaifanya taa yangu iendelee kuwaka; Mungu wangu hulifanya giza langu kuwa mwanga.
כי-אתה תאיר נרי יהוה אלהי יגיה חשכי
29 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
כי-בך ארץ גדוד ובאלהי אדלג-שור
30 Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu, neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
האל תמים דרכו אמרת-יהוה צרופה מגן הוא לכל החסים בו
31 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
כי מי אלוה מבלעדי יהוה ומי צור זולתי אלהינו
32 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
האל המאזרני חיל ויתן תמים דרכי
33 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
משוה רגלי כאילות ועל במתי יעמידני
34 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
מלמד ידי למלחמה ונחתה קשת-נחושה זרועתי
35 Hunipa ngao yako ya ushindi, nao mkono wako wa kuume hunitegemeza, unajishusha chini ili kuniinua.
ותתן-לי מגן ישעך וימינך תסעדני וענותך תרבני
36 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
תרחיב צעדי תחתי ולא מעדו קרסלי
37 Niliwafuatia adui zangu na nikawapata, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
ארדוף אויבי ואשיגם ולא-אשוב עד-כלותם
38 Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
אמחצם ולא-יכלו קום יפלו תחת רגלי
39 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
ותאזרני חיל למלחמה תכריע קמי תחתי
40 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
ואיבי נתתה לי ערף ומשנאי אצמיתם
41 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
ישועו ואין-מושיע על-יהוה ולא ענם
42 Niliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo; niliwamwaga nje kama tope barabarani.
ואשחקם כעפר על-פני-רוח כטיט חוצות אריקם
43 Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu; umenifanya kuwa kiongozi wa mataifa, watu ambao sikuwajua wananitumikia.
תפלטני מריבי-עם תשימני לראש גוים עם לא-ידעתי יעבדוני
44 Mara wanisikiapo hunitii, wageni hunyenyekea mbele yangu.
לשמע אזן ישמעו לי בני-נכר יכחשו-לי
45 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
בני-נכר יבלו ויחרגו ממסגרותיהם
46 Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu Mwokozi wangu!
חי-יהוה וברוך צורי וירום אלוהי ישעי
47 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, awatiishaye mataifa chini yangu,
האל--הנותן נקמות לי וידבר עמים תחתי
48 aniokoaye na adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
מפלטי מאיבי אף מן-קמי תרוממני מאיש חמס תצילני
49 Kwa hiyo nitakusifu katikati ya mataifa, Ee Bwana; nitaliimbia sifa jina lako.
על-כן אודך בגוים יהוה ולשמך אזמרה
50 Humpa mfalme wake ushindi mkuu, huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.
מגדל ישועות מלכו ועשה חסד למשיחו--לדוד ולזרעו עד-עולם

< Zaburi 18 >