< Zaburi 18 >
1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana aliyomwimbia Bwana wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli. Alisema hivi: Nakupenda wewe, Ee Bwana, nguvu yangu.
I will love you, O LORD, my strength.
2 Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu, Mungu wangu ni mwamba, ambaye kwake ninakimbilia. Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu, ngome yangu.
The LORD is my rock, and my fortress, and my deliverer; my God, my strength, in whom I will trust; my buckler, and the horn of my salvation, and my high tower.
3 Ninamwita Bwana anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
I will call upon the LORD, who is worthy to be praised: so shall I be saved from mine enemies.
4 Kamba za mauti zilinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
The sorrows of death compassed me, and the floods of ungodly men made me afraid.
5 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol )
The sorrows of hell compassed me about: the snares of death prevented me. (Sheol )
6 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu anisaidie. Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika mbele zake, masikioni mwake.
In my distress I called upon the LORD, and cried unto my God: he heard my voice out of his temple, and my cry came before him, even into his ears.
7 Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya milima ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Then the earth shook and trembled; the foundations also of the hills moved and were shaken, because he was angry.
8 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
There went up a smoke out of his nostrils, and fire out of his mouth devoured: coals were kindled by it.
9 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
He bowed the heavens also, and came down: and darkness was under his feet.
10 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
And he rode upon a cherub, and did fly: yea, he did fly upon the wings of the wind.
11 Alifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika, hema lake kumzunguka, mawingu meusi ya mvua ya angani.
He made darkness his secret place; his pavilion round about him were dark waters and thick clouds of the skies.
12 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
At the brightness that was before him his thick clouds passed, hail stones and coals of fire.
13 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
The LORD also thundered in the heavens, and the Highest gave his voice; hail stones and coals of fire.
14 Aliipiga mishale yake na kutawanya adui, naam, umeme mwingi wa radi na kuwafukuza.
Yea, he sent out his arrows, and scattered them; and he shot out lightnings, and humiliated them.
15 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwako, Ee Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwako.
Then the channels of waters were seen, and the foundations of the world were discovered at your rebuke, O LORD, at the blast of the breath of your nostrils.
16 Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
He sent from above, he took me, he drew me out of many waters.
17 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
He delivered me from my strong enemy, and from them which hated me: for they were too strong for me.
18 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
They prevented me in the day of my calamity: but the LORD was my stay.
19 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
He brought me forth also into a large place; he delivered me, because he delighted in me.
20 Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
The LORD rewarded me according to my righteousness; according to the cleanness of my hands has he recompensed me.
21 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
For I have kept the ways of the LORD, and have not wickedly departed from my God.
22 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
For all his judgments were before me, and I did not put away his statutes from me.
23 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
I was also upright before him, and I kept myself from mine iniquity.
24 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu machoni pake.
Therefore has the LORD recompensed me according to my righteousness, according to the cleanness of my hands in his eyesight.
25 Kwa yeye aliye mwaminifu, unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia, unajionyesha kutokuwa na hatia.
With the merciful you will show yourself merciful; with an upright man you will show yourself upright;
26 Kwa aliye mtakatifu, unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka, unajionyesha kuwa mkaidi.
With the pure you will show yourself pure; and with the perverse you will show yourself perverse.
27 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini huwashusha wenye kiburi.
For you will save the afflicted people; but will bring down high looks.
28 Wewe, Ee Bwana, unaifanya taa yangu iendelee kuwaka; Mungu wangu hulifanya giza langu kuwa mwanga.
For you will light my candle: the LORD my God will enlighten my darkness.
29 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
For by you I have run through a troop; and by my God have I leaped over a wall.
30 Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu, neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
As for God, his way is perfect: the word of the LORD is tried: he is a buckler to all those that trust in him.
31 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
For who is God save the LORD? or who is a rock save our God?
32 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
It is God that girds me with strength, and makes my way perfect.
33 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
He makes my feet like hinds' feet, and sets me upon my high places.
34 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
He teaches my hands to war, so that a bow of steel is broken by mine arms.
35 Hunipa ngao yako ya ushindi, nao mkono wako wa kuume hunitegemeza, unajishusha chini ili kuniinua.
You have also given me the shield of your salvation: and your right hand has held me up, and your gentleness has made me great.
36 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
You have enlarged my steps under me, that my feet did not slip.
37 Niliwafuatia adui zangu na nikawapata, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
I have pursued mine enemies, and overtaken them: neither did I return till they were consumed.
38 Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
I have wounded them that they were not able to rise: they are fallen under my feet.
39 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
For you have girded me with strength unto the battle: you have subdued under me those that rose up against me.
40 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
You have also given me the necks of mine enemies; that I might destroy them that hate me.
41 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
They cried, but there was none to save them: even unto the LORD, but he answered them not.
42 Niliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo; niliwamwaga nje kama tope barabarani.
Then did I beat them small as the dust before the wind: I did cast them out as the dirt in the streets.
43 Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu; umenifanya kuwa kiongozi wa mataifa, watu ambao sikuwajua wananitumikia.
You have delivered me from the strivings of the people; and you have made me the head of the heathen: a people whom I have not known shall serve me.
44 Mara wanisikiapo hunitii, wageni hunyenyekea mbele yangu.
As soon as they hear of me, they shall obey me: the strangers shall submit themselves unto me.
45 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
The strangers shall fade away, and be afraid out of their close places.
46 Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu Mwokozi wangu!
The LORD lives; and blessed be my rock; and let the God of my salvation be exalted.
47 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, awatiishaye mataifa chini yangu,
It is God that avenges me, and subdues the people under me.
48 aniokoaye na adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
He delivers me from mine enemies: yea, you lift me up above those that rise up against me: you have delivered me from the violent man.
49 Kwa hiyo nitakusifu katikati ya mataifa, Ee Bwana; nitaliimbia sifa jina lako.
Therefore will I give thanks unto you, O LORD, among the heathen, and sing praises unto your name.
50 Humpa mfalme wake ushindi mkuu, huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.
Great deliverance gives he to his king; and shows mercy to his anointed, to David, and to his seed for evermore.