< Zaburi 17 >

1 Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
Molitev Davidova: Čuj, Gospod, pravico, poslušaj vpitje moje; uho nagni molitvi moji brez ustnic zvijačnih.
2 Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
Od obličja tvojega izidi pravica moja; oči tvoje naj gledajo, kar je pravično.
3 Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
Ko bodeš preiskal srce moje, obiskal ponoči, preskušal me, ne najdeš; kar mislim, ne prestopi mojih ust.
4 Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
Pri delih človeških, po besedi ustnic tvojih opazujem steze silovitega.
5 Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
Ohrani korake moje na stezah svojih, da ne zaidejo moje noge.
6 Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
Jaz te kličem, ker me slišiš, Bog mogočni; nagni k meni uho svoje, poslušaj govor moj.
7 Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
Odloči milosti svoje, o ti, ki otimaš preganjalcev pribegajoče na desnico tvojo.
8 Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
Hrani me kakor zenico v očesu; sè senco peroti svojih skrivaj me:
9 kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
Zaradi krivičnih, ki me napadajo, sovražnikov mojih glavnih, ki me obdajajo.
10 Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
Mast svojo masté, z usti svojimi govoré prevzetno:
11 Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
Hojo našo zdaj obdajajo nam; oči svoje obračajo vpirajoč v tla.
12 Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
Podoba je vsakega kakor leva želečega zgrabiti, in kakor mladega leva čepečega v zakotji.
13 Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
Vstani, Gospod, prehítí obličje njegovo; trešči ga, izpuli dušo mojo z mečem svojim krivičnemu.
14 Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
Ljudém izpuli v roko svojo, Gospod, ljudém od svetá, katerih delež je v tem življenji, katerim trebuh polniš sè skrivnim zakladom svojim; sitijo se sinovi in preobilost svojo zapuščajo otrokom svojim.
15 Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.
Jaz bodem v pravičnosti videl obličje tvoje, sitil se bodem, ko se zbudim, s podobo tvojo.

< Zaburi 17 >