< Zaburi 17 >

1 Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
Oratio David. Exaudi Domine iustitiam meam: intende deprecationem meam. Auribus percipe orationem meam, non in labiis dolosis.
2 Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
De vultu tuo iudicium meum prodeat: oculi tui videant æquitates.
3 Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
Probasti cor meum, et visitasti nocte: igne me examinasti, et non est inventa in me iniquitas.
4 Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
Ut non loquatur os meum opera hominum: propter verba labiorum tuorum ego custodivi vias duras.
5 Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
Perfice gressus meos in semitis tuis: ut non moveantur vestigia mea.
6 Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
Ego clamavi, quoniam exaudisti me Deus: inclina aurem tuam mihi, et exaudi verba mea.
7 Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
Mirifica misericordias tuas, qui salvos facis sperantes in te.
8 Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
A resistentibus dexteræ tuæ custodi me, ut pupillam oculi. Sub umbra alarum tuarum protege me:
9 kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
a facie impiorum qui me afflixerunt. Inimici mei animam meam circumdederunt,
10 Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
adipem suum concluserunt: os eorum locutum est superbiam.
11 Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
Proiicientes me nunc circumdederunt me: oculos suos statuerunt declinare in terram.
12 Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
Susceperunt me sicut leo paratus ad prædam: et sicut catulus leonis habitans in abditis.
13 Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
Exurge Domine, præveni eum, et supplanta eum: eripe animam meam ab impio, frameam tuam ab inimicis manus tuæ.
14 Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
Domine a paucis de terra divide eos in vita eorum: de absconditis tuis adimpletus est venter eorum. Saturati sunt filiis: et dimiserunt reliquias suas parvulis suis.
15 Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.
Ego autem in iustitia apparebo conspectui tuo: satiabor cum apparuerit gloria tua.

< Zaburi 17 >