< Zaburi 17 >

1 Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
Accogli, Signore, la causa del giusto, sii attento al mio grido. Porgi l'orecchio alla mia preghiera: sulle mie labbra non c'è inganno. Preghiera. Di Davide.
2 Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
Venga da te la mia sentenza, i tuoi occhi vedano la giustizia.
3 Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
Saggia il mio cuore, scrutalo di notte, provami al fuoco, non troverai malizia. La mia bocca non si è resa colpevole,
4 Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
secondo l'agire degli uomini; seguendo la parola delle tue labbra, ho evitato i sentieri del violento.
5 Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
Sulle tue vie tieni saldi i miei passi e i miei piedi non vacilleranno.
6 Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
Io t'invoco, mio Dio: dammi risposta; porgi l'orecchio, ascolta la mia voce,
7 Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
mostrami i prodigi del tuo amore: tu che salvi dai nemici chi si affida alla tua destra.
8 Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
Custodiscimi come pupilla degli occhi, proteggimi all'ombra delle tue ali,
9 kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
di fronte agli empi che mi opprimono, ai nemici che mi accerchiano.
10 Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
Essi hanno chiuso il loro cuore, le loro bocche parlano con arroganza.
11 Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
Eccoli, avanzano, mi circondano, puntano gli occhi per abbattermi;
12 Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
simili a un leone che brama la preda, a un leoncello che si apposta in agguato.
13 Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
Sorgi, Signore, affrontalo, abbattilo; con la tua spada scampami dagli empi,
14 Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
con la tua mano, Signore, dal regno dei morti che non hanno più parte in questa vita. Sazia pure dei tuoi beni il loro ventre se ne sazino anche i figli e ne avanzi per i loro bambini.
15 Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.
Ma io per la giustizia contemplerò il tuo volto, al risveglio mi sazierò della tua presenza.

< Zaburi 17 >