< Zaburi 17 >
1 Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
Une prière de David. Écoute, Yahvé, mon juste plaidoyer. Prêtez l'oreille à ma prière qui ne sort pas de lèvres trompeuses.
2 Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
Que ma sentence sorte de ta présence. Que vos yeux regardent l'équité.
3 Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
Tu as éprouvé mon cœur. Tu m'as rendu visite dans la nuit. Vous m'avez jugé, et n'avez rien trouvé. J'ai résolu que ma bouche ne désobéirait pas.
4 Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
Quant aux actes des hommes, par la parole de tes lèvres, Je me suis tenu à l'écart des voies de la violence.
5 Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
Mes pas se sont attachés à tes sentiers. Mes pieds n'ont pas glissé.
6 Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
J'ai fait appel à toi, car tu me répondras, Dieu. Tourne ton oreille vers moi. Écoutez mon discours.
7 Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
Montre ta merveilleuse bonté, toi qui sauves de leurs ennemis ceux qui se réfugient par ta droite.
8 Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
Garde-moi comme la prunelle de tes yeux. Cache-moi à l'ombre de tes ailes,
9 kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
des méchants qui m'oppriment, mes ennemis mortels, qui m'entourent.
10 Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
Ils ferment leurs cœurs insensibles. Avec leur bouche, ils parlent fièrement.
11 Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
Ils nous ont maintenant entourés sur nos pas. Ils se sont mis en tête de nous jeter à terre.
12 Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
Il est comme un lion qui est avide de sa proie, comme un jeune lion à l'affût dans les endroits secrets.
13 Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
Lève-toi, Yahvé, confronte-le. Rejetez-le. Délivre mon âme des méchants par ton épée,
14 Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
des hommes par ta main, Yahvé, des hommes du monde, dont la part est dans cette vie. Vous remplissez le ventre de ceux que vous aimez. Vos fils en ont plein, et ils accumulent des richesses pour leurs enfants.
15 Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.
Quant à moi, je verrai ta face dans la justice. Je me contenterai, à mon réveil, de voir votre forme.