< Zaburi 17 >

1 Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
The preier of Dauid. Lord, here thou my riytfulnesse; biholde thou my preier. Perseuye thou with eeris my preier; not maad in gileful lippis.
2 Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
Mi doom come `forth of thi cheer; thin iyen se equite.
3 Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
Thou hast preued myn herte, and hast visitid in niyt; thou hast examynyd me bi fier, and wickidnesse is not foundun in me.
4 Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
That my mouth speke not the werkis of men; for the wordis of thi lippis Y haue kept harde weies.
5 Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
Make thou perfit my goyngis in thi pathis; that my steppis be not moued.
6 Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
I criede, for thou, God, herdist me; bowe doun thin eere to me, and here thou my wordis.
7 Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
Make wondurful thi mercies; that makist saaf `men hopynge in thee.
8 Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
Kepe thou me as the appil of the iye; fro `men ayenstondynge thi riyt hond. Keuere thou me vndur the schadewe of thi wyngis;
9 kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
fro the face of vnpitouse men, that han turmentid me. Myn enemyes han cumpassid my soule;
10 Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
thei han closide togidere her fatnesse; the mouth of hem spak pride.
11 Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
Thei castiden me forth, and han cumpassid me now; thei ordeyneden to bowe doun her iyen in to erthe.
12 Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
Thei, as a lioun maad redi to prey, han take me; and as the whelp of a lioun dwellynge in hid places.
13 Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
Lord, rise thou vp, bifor come thou hym, and disseyue thou hym; delyuere thou my lijf fro the `vnpitouse,
14 Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
delyuere thou thi swerd fro the enemyes of thin hond. Lord, departe thou hem fro a fewe men of `the lond in the lijf of hem; her wombe is fillid of thin hid thingis. Thei ben fillid with sones; and thei leften her relifis to her litle children.
15 Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.
But Y in riytfulnesse schal appere to thi siyt; Y schal be fillid, whanne thi glorie schal appere.

< Zaburi 17 >