< Zaburi 17 >

1 Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
A Prayer of David. Hear the right, O LORD, attend to my cry, give ear to my prayer, [that goeth] not out of feigned lips.
2 Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
Let my sentence come forth from thy presence; let thy eyes behold the things that are equal.
3 Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
Thou hast proved my heart; thou hast visited [me] in the night; thou hast tried me, [and] shalt find nothing; I have purposed [that] my mouth shall not transgress.
4 Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
Concerning the works of men, by the word of thy lips I have kept [me from] the paths of the destroyer.
5 Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
Uphold my goings in thy paths, [that] my footsteps slip not.
6 Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
I have called upon thee, for thou wilt hear me, O God: incline thy ear to me, [and hear] my speech.
7 Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
Show thy wonderful loving-kindness, O thou that savest by thy right hand them who put their trust [in thee] from those that rise up [against them].
8 Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
Keep me as the apple of the eye, hide me under the shade of thy wings.
9 kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
From the wicked that oppress me, [from] my deadly enemies, [who] encompass me,
10 Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
They are inclosed in their own fat: with their mouth they speak proudly.
11 Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
They have now compassed us in our steps: they have set their eyes bowing down to the earth;
12 Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
Like as a lion [that] is greedy of his prey, and as it were a young lion lurking in secret places.
13 Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
Arise, O LORD disappoint him, cast him down: deliver my soul from the wicked, [who is] thy sword:
14 Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
From men [who are] thy hand, O LORD, from men of the world, [who have] their portion in [this] life, and whose belly thou fillest with thy hid [treasure]: they are full of children, and leave the rest of their [substance] to their babes.
15 Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.
As for me, I shall behold thy face in righteousness: I shall be satisfied, when I awake, with thy likeness.

< Zaburi 17 >