< Zaburi 17 >
1 Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
A prayer of David. Listen, O Lord, to my innocence; attend to my piercing cry. Give heed to my prayer out of lips unfeigned.
2 Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
Let my vindication come from you, your eyes see the truth.
3 Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
When you test my heart when you visit at night, and assay me like silver – you can find no evil. I am determined that my mouth should not lie.
4 Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
I gave earnest heed to the words of your lips.
5 Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
My steps have held fast to the paths of your precepts and in your tracks have my feet never stumbled.
6 Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
So I call you, O God, with assurance of answer; bend down your ear to me, hear what I say.
7 Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
Show your marvelous love, you who save from enemies those who take refuge at your right hand.
8 Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
Keep me as the apple of the eye, hide me in the shelter of your wings.
9 kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
From wicked people who do me violence, from deadly foes who crowd around me.
10 Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
They have closed their hearts to pity, the words of their mouths are haughty.
11 Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
Now they dog us at every step, keenly watching, to hurl us to the ground,
12 Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
like a lion, longing to tear, like a young lion, lurking in secret.
13 Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
Arise, Lord, face them and fell them. By your sword set me free from the wicked,
14 Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
by your hand, O Lord, from those – whose portion of life is but of this world. But let your treasured ones have food in plenty may their children be full and their children satisfied.
15 Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.
In my innocence I will see your face, awake I am filled with a vision of you.