< Zaburi 17 >

1 Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
A PRAYER OF DAVID. Hear, O YHWH, righteousness, attend my cry, Give ear [to] my prayer, without lips of deceit.
2 Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
My judgment goes out from before You; Your eyes see uprightly.
3 Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
You have proved my heart, You have inspected by night, You have tried me, You find nothing; My thoughts do not pass over my mouth.
4 Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
As for doings of man, Through a word of Your lips I have observed The paths of a destroyer;
5 Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
To uphold my goings in Your paths, My steps have not slipped.
6 Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
I called You, for You answer me, O God, incline Your ear to me, hear my speech.
7 Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
Separate Your kindness wonderfully, O Savior of the confiding, By Your right hand, from withstanders.
8 Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
Keep me as the apple, the daughter of the eye; Hide me in the shadow of Your wings,
9 kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
From the face of the wicked who spoiled me, [From] my enemies in soul who go around against me.
10 Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
They have closed up their fat, Their mouths have spoken with pride:
11 Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
“Our steps have now surrounded [him]”; They set their eyes to turn aside in the land.
12 Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
His likeness as a lion desirous to tear, As a young lion dwelling in secret places.
13 Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
Arise, O YHWH, go before his face, Cause him to bend. Deliver my soul from the wicked, Your sword,
14 Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
From men, Your hand, O YHWH, From men of the world, their portion [is] in life, And [with] Your hidden things You fill their belly, They are satisfied [with] sons, And have left their abundance to their sucklings.
15 Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.
I—in righteousness, I see Your face; I am satisfied, in awaking, [with] Your form!

< Zaburi 17 >