< Zaburi 17 >

1 Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
The prayer of Dauid. Heare the right, O Lord, consider my crye: hearken vnto my prayer of lips vnfained.
2 Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
Let my sentence come forth from thy presence, and let thine eyes beholde equitie.
3 Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
Thou hast prooued and visited mine heart in the night: thou hast tryed me, and foundest nothing: for I was purposed that my mouth should not offend.
4 Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
Concerning the workes of men, by the wordes of thy lips I kept mee from the paths of the cruell man.
5 Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
Stay my steps in thy paths, that my feete doe not slide.
6 Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
I haue called vpon thee: surely thou wilt heare me, O God: incline thine eare to me, and hearken vnto my wordes.
7 Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
Shewe thy marueilous mercies, thou that art the Sauiour of them that trust in thee, from such as resist thy right hand.
8 Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
Keepe me as the apple of the eye: hide me vnder the shadowe of thy wings,
9 kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
From the wicked that oppresse mee, from mine enemies, which compasse me round about for my soule.
10 Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
They are inclosed in their owne fat, and they haue spoken proudely with their mouth.
11 Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
They haue compassed vs now in our steps: they haue set their eyes to bring downe to the ground:
12 Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
Like as a lyon that is greedy of pray, and as it were a lyons whelp lurking in secret places.
13 Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
Vp Lord, disappoint him: cast him downe: deliuer my soule from the wicked with thy sworde,
14 Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
From men by thine hand, O Lord, from men of the world, who haue their portion in this life, whose bellies thou fillest with thine hid treasure: their children haue ynough, and leaue the rest of their substance for their children.
15 Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.
But I will beholde thy face in righteousnes, and when I awake, I shalbe satisfied with thine image.

< Zaburi 17 >