< Zaburi 17 >
1 Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
A prayer of David. Lord, please hear my cry for justice! Please pay attention to my call for help! Listen to the prayer of an honest man!
2 Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
Vindicate me before you—for you see what is right.
3 Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
You have observed my thoughts, you have visited me at night, you have examined me—and you have found nothing wrong. I promised myself I wouldn't say anything I shouldn't.
4 Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
With regard to the actions of others: I have done what you told me and I have avoided what violent people do.
5 Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
I have not strayed from your path; my feet have not slipped from it.
6 Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
God, I call out to you because I know you will answer; please listen carefully to what I have to say.
7 Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
Show me how wonderful your trustworthy love really is, Savior of those who come to you for protection against their enemies!
8 Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
Keep me safe as someone you love; hide me underneath your wings.
9 kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
Protect me from the attacks of the wicked who want to destroy me, from my enemies who surround me, intent on killing me.
10 Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
They have no compassion, and all they have to say is pure arrogance.
11 Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
They hunt me down and surround me, looking for the chance to knock me down in the dust.
12 Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
They are like lions, longing to tear their prey apart; like fierce lions crouching in ambush.
13 Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
Lord, stand up and confront them! Force them to back down! By your sword rescue me from the wicked!
14 Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
Lord, by your power, save me from people whose only thought is for this world. May they be filled with what you have in store for them, their children too, with left-overs for their grandchildren!
15 Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.
As for me, I shall see your face in all its goodness. When I awake, I will be so pleased to see you face to face.