< Zaburi 17 >

1 Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
The prayer of David. Hear, O Lord, my justice: attend to my supplication. Give ear unto my prayer, which proceedeth not from deceitful lips.
2 Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
Let my judgment come forth from thy countenance: let thy eyes behold the things that are equitable.
3 Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
Thou hast proved my heart, and visited it by night, thou hast tried me by fire: and iniquity hath not been found in me.
4 Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
That my mouth may not speak the works of men: for the sake of the words of thy lips, I have kept hard ways.
5 Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
Perfect thou my goings in thy paths: that my footsteps be not moved.
6 Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
I have cried to thee, for thou, O God, hast heard me: O incline thy ear unto me, and hear my words.
7 Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
Shew forth thy wonderful mercies; thou who savest them that trust in thee.
8 Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
From them that resist thy right hand keep me, as the apple of thy eye. Protect me under the shadow of thy wings.
9 kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
From the face of the wicked who have afflicted me. My enemies have surrounded my soul:
10 Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
They have shut up their fat: their mouth hath spoken proudly.
11 Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
They have cast me forth and now they have surrounded me: they have set their eyes bowing down to the earth.
12 Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
They have taken me, as a lion prepared for the prey; and as a young lion dwelling in secret places.
13 Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
Arise, O Lord, disappoint him and supplant him; deliver my soul from the wicked one: thy sword
14 Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
From the enemies of thy hand. O Lord, divide them from the few of the earth in their life: their belly is filled from thy hidden stores. They are full of children: and they have left to their little ones the rest of their substance.
15 Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.
But as for me, I will appear before thy sight in justice: I shall be satisfied when thy glory shall appear.

< Zaburi 17 >