< Zaburi 17 >

1 Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
A prayer of David. Hearken, O Lord of my righteousness, attend to my petition; give ear to my prayer not [uttered] with deceitful lips.
2 Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
Let my judgment come forth from thy presence; let mine eyes behold righteousness.
3 Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
Thou has proved mine heart; thou hast visited [me] by night; thou hast tried me as with fire, and unrighteousness has not been found in me: [I am purposed] that my mouth shall not speak [amiss].
4 Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
As for the works of men, by the words of thy lips I have guarded [myself from] hard ways.
5 Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
Direct my steps in thy paths, that my steps slip not.
6 Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
I have cried, for thou heardest me, O God: incline thine ear to me, and hearken to my words.
7 Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
Shew the marvels of thy mercies, thou that savest them that hope in thee.
8 Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
Keep me as the apple of the eye from those that resist thy right hand: thou shalt screen me by the covering of thy wings,
9 kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
from the face of the ungodly that have afflicted me: mine enemies have compassed about my soul.
10 Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
They have enclosed [themselves with] their own fat: their mouth has spoken pride.
11 Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
They have now cast me out and compassed me round about: they have set their eyes [so as] to bow them down to the ground.
12 Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
They laid wait for me as a lion ready for prey, and like a lion's whelp dwelling in secret [places].
13 Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
Arise, O Lord, prevent them, and cast them down: deliver my soul from the ungodly: [draw] thy sword,
14 Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
because of the enemies of thine hand: O Lord, destroy them from the earth; scatter them in their life, though their belly has been filled with thy hidden [treasures]: they have been satisfied with uncleanness, and have left the remnant [of their possessions] to their babes.
15 Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.
But I shall appear in righteousness before thy face: I shall be satisfied when thy glory appears.

< Zaburi 17 >