< Zaburi 17 >

1 Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
A prayer of David. Hear, O LORD, my righteous plea; listen to my cry. Give ear to my prayer— it comes from lips free of deceit.
2 Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
May my vindication come from Your presence; may Your eyes see what is right.
3 Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
You have tried my heart; You have visited me in the night. You have tested me and found no evil; I have resolved not to sin with my mouth.
4 Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
As for the deeds of men— by the word of Your lips I have avoided the ways of the violent.
5 Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
My steps have held to Your paths; my feet have not slipped.
6 Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
I call on You, O God, for You will answer me. Incline Your ear to me; hear my words.
7 Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
Show the wonders of Your loving devotion, You who save by Your right hand those who seek refuge from their foes.
8 Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
Keep me as the apple of Your eye; hide me in the shadow of Your wings
9 kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
from the wicked who assail me, from my mortal enemies who surround me.
10 Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
They have closed their callous hearts; their mouths speak with arrogance.
11 Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
They have tracked us down, and now surround us; their eyes are set to cast us to the ground,
12 Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
like a lion greedy for prey, like a young lion lurking in ambush.
13 Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
Arise, O LORD, confront them! Bring them to their knees; deliver me from the wicked by Your sword,
14 Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
from such men, O LORD, by Your hand— from men of the world whose portion is in this life. May You fill the bellies of Your treasured ones and satisfy their sons, so they leave their abundance to their children.
15 Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.
As for me, I will behold Your face in righteousness; when I awake, I will be satisfied in Your presence.

< Zaburi 17 >