< Zaburi 17 >
1 Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
Hear the right, O Jehovah, attend to my cry. Give ear to my prayer, that goes not out of feigned lips.
2 Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
Let my justice come forth from thy presence. Let thine eyes look upon equity.
3 Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
Thou have proved my heart. Thou have visited me in the night. Thou have tried me, and find nothing. I have purposed that my mouth shall not transgress.
4 Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
As for the works of men, by the word of thy lips I have kept from the ways of a violent man.
5 Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
My steps have held fast to thy paths. My feet have not slipped.
6 Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
I have called upon thee, for thou will answer me, O God. Incline thine ear to me, and hear my speech.
7 Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
Show thy marvelous loving kindness, O thou who saves by thy right hand those who take refuge from those who rise up.
8 Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
Keep me as the apple of the eye. Hide me under the shadow of thy wings,
9 kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
from the wicked who oppress me, my deadly enemies, who encompass me around.
10 Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
They are enclosed in their own fat. With their mouth they speak proudly.
11 Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
They have now encompassed us in our steps. They set their eyes to cast down to the earth.
12 Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
He is like a lion that is greedy of his prey, and as it were a young lion lurking in secret places.
13 Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
Arise, O Jehovah, confront him. Cast him down. Deliver my soul from the wicked by thy sword,
14 Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
from men by thy hand, O Jehovah, from men of the world whose portion is in this life, and whose belly thou fill with thy treasure. They are satisfied with sons, and leave the rest of their substance to their babes.
15 Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.
As for me, I shall behold thy face in righteousness. I shall be satisfied, when I awake, with thy form.